Mkurugenzi
wa Sanaa kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi.
Leah Kihimbi akimkabidhi bendera ya Taifa mshiriki wa mashindano ya Miss
Word Super Model 2017, Miss. Asha Ally Mabula (kushoto) wakati wa hafla
ya kumkabidhi bendera hiyo iliyofanyika katika Ukumbi wa Idara ya
Habari – MAELEZO leo Jijini Dar es Salaam. Miss huyo anatarajia kuondoka
nchini leo kuelekea Macau nchini China ambapo atashiriki mashindano
hayo. Katikati ni Afisa Utumishi wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA).
Baadhi
ya waandishi wa habari wakishuhudia tukio la kumkabidhi bendera ya
Taifa mshiriki wa Miss Word Super Model, Asha Ally Mabula anayetarajia
kushiriki mashindano hayo Macau nchini China.
Mkurugenzi
wa Sanaa kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi.
Leah Kihimbi akizungumza wakati wa tukio la kumkabidhi bendera ya Taifa
mshiriki wa mashindano ya Miss Word Super Model 2017, Miss. Asha Ally
Mabula (kushoto) leo Jijini Dar es Salaam. Miss huyo anatarjia kuondoka
leo kuelekea Macau nchini China ambapo atashiriki mashindano hayo.
Miss
Super Model 2017 Asha Ally Mabula akizungumza wakati wa tukio la
kukabidhiwa bendera ya Taifa kwa ajili ya kuiwakilisha nchi katika
mashindano ya Miss Word Super Model 2017 leo Jijini Dar es Salaam. Miss
huyo anatarajia kuondoka leo kuelekea Macau nchini China ambapo
atashiriki mashindano hayo. Kutoka kulia ni Afisa Utumishi wa Baraza la
Sanaa la Taifa (BASATA), Mkurugenzi wa Sanaa kutoka Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Leah Kihimbi na Meneja Mkuu wa
Tanzania Miss Super Model Ibrahim Thabit.
Picha na: Frank Shija – MAELEZO.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...