Frank Mvungi-Maelezo

Serikali imewahakikishia wananchi kuwa dawa zilizopo katika soko zina ubora kwa asilimia 98 na itahakiksha zinaendelea kukidhi vigezo vya ubora kama zilivyokuwa wakati zinasajiliwa kwa mujibu wa sheria, kanuni,miongozo na taratibu za udhibiti.

Kauli hiyo imetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya chakula na Dawa (TFDA) Bw. Hiiti Sillo wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliolenga kueleza mikakati ya Mamlaka hiyo katika kudhibiti ubora na usalama wa chakula,dawa,vipodozi na vifaa tiba ili kulinda afya za wananchi.

“Katika maabara ya TFDA inayokidhi ithibati ya Shirika la Afya Duniani (WHO) kati ya sampuli za dawa 199 za Binadamu zilizochunguzwa,sampuli 184 sawa na asilimia 92.5 zilikidhi vigezo vya ubora na sampuli za dawa 10 aina ya Ergometrine ya sindano ambayo ni sampuli 5 sawa na asilimia 2.5 hazikufikia ubora kwa kuwa na kiasi cha kiambata hai chini ya kiwango kinachokubalika.”Alisisitiza Sillo

Akifafanua Sillo amesema kabla ya dawa kusajiliwa na TFDA na hatimaye kuruhusiwa kuingia katika Soko,zinafanyiwa tathmini ya Ubora,Usalama na ufanisi sanjari na ukaguzi wa mifumo ya utengenezaji bora Kiwandani na hizo ni hatua za awali za mifumo ya udhibiti wa dawa duniani.

Pia Sillo aliongeza kuwa dawa zinapokuwa katika soko zinafuatiliwa na TFDA kuona kama zinaendelea kukidhi vigezo vya ubora hadi tarehe ya mwisho ya matumizi (expiry date) ambapo utaratibu huu hujulikana kama Post- Marketing Surveillance au Market Control kwa mujibu wa mwongozo wa shirika la Afya Duniani (WHO) na ulianza kuwekwa na TFDA tangu mwaka 2007.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) Hiiti Sillo akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Taasisi yake leo Jijini Dar es Salaam.
: Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) Hiiti Sillo akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Taasisi yake leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Meneja Majaribio ya Dawa na Ufuatiliaji kutoka Mamlaka hiyo Bi. Kissa Mwamwitwa.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) Hiiti Sillo (katikati) akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari wakati wa mkutano wake na waandishi wahabari( hawapo pichani) kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Taasisi yake leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Meneja wa Kanda ya Mashariki wa TFDA, Emmanuel Alphonce na Meneja Majaribio ya Dawa na Ufuatiliaji kutoka Mamlaka hiyo Bi. Kissa Mwamwitwa.Picha zote na: Frank Mvungi – MAELEZO.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...