Timu
ya Wilaya ya UMISETA imekabidhiwa bendera ya michezo ya Wilaya na
kutakiwa kwenda kuiwakilisha wilaya kwenye mashindano ya UMISETA kwenye
ngazi ya Mkoa ambayo yatafanyikia wilayani Geita.
Akiongea wakati wa kufunga mashindano ya UMISETA ngazi ya Wilaya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe Elias Kayandabila amewataka wanamichezo hao wakacheze kwa bidii na maarifa ili walete ushindi wilayani kwetu
Pamoja na hayo Mkurugenzi amewataka wakawe na nidhamu ya hali ya juu kwani michezo inahitaji nidhamu na kujituma.
Kaimu Afisa Elimu Sekondari bi Exvaria Mlowe amemshukuru Mkurugenzi kwa kuiwezesha timu ya wilaya kufanikiwa kwenye maandalizi ya UMISETA ngazi ya Wilaya.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mbogwe ndg Elias Kayandabila akionge na timu ya UMISETA ya Wilaya wakati akifunga mashindano hayo kwa ngazi ya wilaya.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashuri ya Mbogwe Ndg Elias kayandabila akiwakabidhi wanamichezo bendera ya michezo ya Wilaya
Timu ya Wilaya ya UMISETA imekabidhiwa bendera ya michezo ya Wilaya na kutakiwa kwenda kuiwakilisha wilaya kwenye mashindano ya UMISETA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...