Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO.
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
imetoa somo la masuala ya kodi kwa wafanyabiashara kutoka China
wanaoishi nchini kwa lengo la kuwaongezea uelewa juu ya sheria na
taratibu za ulipaji kodi katika semina kuhusu mafunzo hayo leo Jijini
Dar es Salaam.
Akiwasilisha mada wakati wa
mafunzo hayo, Meneja wa Idara ya Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi wa TRA,
Gabriel Mwangosi amesema kuwa Tanzania ya sasa ina fursa nyingi za
uwekezaji hivyo wafanyabiashara hao watakapokuja kuwekeza lazima
wafahamu kanuni na taratibu za ulipaji kodi nchini ili waweze kuendana
na sheria zilizopangwa na nchini.
“Semina hii mahususi imeandaliwa
kwa ajili ya wafanyabiashara wa kichina wanaoishi nchini kupata mafunzo
ya kodi zikiwemo za zuio, majengo pamoja na ushuru na forodha ambazo ni
lazima wazifahamu kwa manufaa ya Taifa letu na wao pia,”alisema
Mwangosi.
Meneja wa Idara ya Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi wa TRA, Gabriel Mwangosi akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu semina juu ya Kodi, Utaratibu na Sheria kwa wafanyabiashara kutoka China iliyoandaliwa kwa ushirikiano wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) pamoja na Kampuni ya Jiteng Consultancy Ltd na kufanyika leo Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa.
Mrakibu wa uhamiaji na Afisa Vibali vya Ukazi, Eliud Ikomba akitoa semina kwa wafanyabiashara kutoka China (hawapo pichani) juu ya sheria za uhamiaji katika semina iliyoandaliwa kwa ushirikiano wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) pamoja na Kampuni ya Jiteng Consultancy Ltd na kufanyika leo Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa.
Baadhi ya wafanyabiashara kutoka China wanaofanya biashara zao nchini wakisikiliza mafunzo mbalimbali juu ya Kodi, Utaratibu na Sheria katika semina iliyoandaliwa kwa ushirikiano wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) pamoja na Kampuni ya Jiteng Consultancy Ltd na kufanyika leo Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...