Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

UCHAGUZI wa viongozi wa Chama cha Makocha wa Mpira wa Miguu (TAFCA) Mkoa wa Kinondoni uliokuwa ufanyike Mei 7 mwaka huu jijini Dar es Salaam sasa umesogezwa mbele hadi Juni 4.


Uamuzi wa kusogeza mbele uchaguzi huo umetokana na mwitikio mdogo wa uchukuaji fomu kwa wagombea. Muda wa uchukuaji fomu sasa umeongezwa hadi Mei 7 mwaka huu.

Fomu kwa ajili ya wagombea zinatolewa kwenye ofisi za Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Kinondoni (KIFA) kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 10 jioni.

Ada ya fomu kwa wagombea wa nafasi za Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu, Katibu Msaidizi na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TAFCA ni sh. 50,000 wakati Mhazini, Mhazini Msaidizi na wajumbe wa Kamati ya Utendaji ni sh. 30,000.

Ajenda ya uchaguzi itatanguliwa na Mkutano Mkuu wa Kawaida ambao mbali ya taarifa ya utendaji, Kamati ya Utendaji inayomaliza muda wake pia itawasilisha ripoti ya mapato na matumizi.

Kamati ya Uchaguzi ya TAFCA Kinondoni inaongozwa na Mwenyekiti wa zamani wa TAFCA, Ramadhan Mambosasa.

Kamati ya Utendaji ya TAFCA Kinondoni inayomaliza muda wake inaongozwa na Mwenyekiti Eliutery Mholery (0715 621 667) na Katibu Mkuu wake Mbwana Makata (0655 520 129).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...