Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilayani
Simanjiro Mkoani Manyara, imeungana na wapenda maendeleo nchini
kumpongeza Rais John Magufuli kwa hatua ya kuzuia usafirishaji mchanga
wa madini (makinikia) nje ya nchi.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Katibu wa UVCCM wilayani
Simanjiro, Bakary Mwacha alisema hatua aliyochukua Rais Magufuli ni ya
kupongezwa na kuungwa mkono na wapenda maendeleo nchini.

Mwacha alisema kitendo hicho kinapaswa kupongezwa kwani kimeonyesha
uzalendo na kulinda rasilimali za nchi na kuchukua hatua kwa viongozi
wazembe waliosababisha hali hiyo.

Alisema Rais Magufuli alipokuwa anatoa ahadi kwa wananchi kipindi
anachoomba kura mwaka 2015, kuwa atakuwa mstari wa mbele kulinda
maslahi ya Taifa ndivyo anavyofanya hivi sasa.“Ni muda mrefu nchi yetu imeibiwa kupitia madini hayo yaliyokuwa yanatoroshwa ila mara baada ya Rais Magufuli kuunda tume na kubaini madudu yaliyopo alikomesha jambo hilo,” alisema.

Hata hivyo, Mwacha alimpongeza Kaimu Katibu wa UVCCM Taifa, Shaka
Hamdu Shaka kwa kutoa tamko la kumtetea na kumlinda kwa gharama yoyote
Rais Magufuli kwa hatua ya kutekeleza mambo ya mabadilikoya kiuchumi
kisiasa na kijamii. “Sisi jumuiya ya UVCCM wilayani Simanjiro tupo bega kwa bega katika kuhakikisha tunatekeleza na kuunga mkono yale yote yanayotamkwa na
viongozi wetu wa UVCCM ngazi ya Taifa,” alisema Mwacha.

Alisema anapongeza jitihada zinazofanywa na Shaka kufanya ziara zake
za kuzunguka nchi nzima na kuzungumza kwenye vikao vya ndani kwani
anaimarisha jumuiya hiyo na kuongeza mshikamano wa vijana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...