Mabalozi wa vijana wanaoiwakilisha Tanzania katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, Yohana Lambo Mayenga pamoja na Suzane William Mollel wamekutana na Wafunzi wa Chuo cha Stella Maris kilichopo Mkoani Mtwara, kwa lengo la kutoa mafunzo na kuwahamasisha Wanafunzi wa vyuo vikuu (Vijana) nchini kote, kuufahamu umuhimu wa Ushirikiano wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na kuuimarisha katika Mchakato wa Jumuiya hiyo Kikanda, katika Warsha ya siku moja iliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo, Mei 12, 2017. Jumla ya Wanafunzi 230 walihudhulia Warsha hiyo.
Mabalozi wa vijana wanaoiwakilisha Tanzania katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, Yohana Lambo Mayenga pamoja na Suzane William Mollel (wa tatu na nne kushoto) wakiwa wameshika Bendera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na baadhi ya Wafunzi wa Chuo cha Stella Maris kilichopo Mkoani Mtwara, wakati wa Warsha ya siku moja iliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo, Mei 12, 2017.
Naibu Balozi wa vijana wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Suzane William Mollel (aliyesimama) akiwasilisha mada katika Warsha ya siku moja kwa Wafunzi wa Chuo cha Stella Maris kilichopo Mkoani Mtwara, juu ya umuhimu wa Ushirikiano wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na kuuimarisha Mchakato wa Jumuiya hiyo Kikanda, iliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo, Mei 12, 2017. 
 Wanafunzi wa Chuo cha Stella Maris kilichopo Mkoani Mtwara, wakimsikiliza kwa makini Balozi wa vijana wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Yohana Lambo Mayenga.
Sehemu ya wanafunzi hao wakiwa kwenye Warsha hiyo.
Balozi wa vijana wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Yohana Lambo Mayenga akikabidhi Stella Maris kilichopo Mkoani Mtwara akikabidhi Bendera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa mmoja wa Viongozi wa Serikali ya Wanafunzi wa chuo hicho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...