Na Mahmoud Ahmad, Globu ya Jamii - Kondoa

Mkuu wa wilaya ya Kondoa Sezaria Makota amewataka waalimu,watendaji na wadau wa elimu wilayani humo kuhakikisha ufaulu wa wanafunzi unavuka lengo walilojiwekea sanjari na kuhakikisha maabara zinakamilika kwa wakati kwenye shule mbalimbali ili vifaa vya maabara walivyoahidiwa na wizara ya elimu wapewe kwa wakati.

Kauli hiyo ameitoa kwenye sherehe za tathmini ya sekta ya elimu wilayani humo iliyofanyika kwenye ukumbi wa Kondoa Irangi.

Amesisitiza kuwa suala la kuwapatia elimu watoto wilayani humo ni jukumu ambalo linahitaji ushirikiano wa wadau wote wa elimu na si suala la walimu pekee hivyo kwa umoja wao wanatakiwa kutoa ushirikiano ili kuweza kufanikiwa kufikia malengo katika sekta hiyo.

“Tumekuwa nyuma katika sekta ya elimu hivyo nawasihi wadau wote kuhakikisha wanafunzi wilayani hapa wanapata huduma muhimu ilikuweza kufikia malengo tarajiwa ya ufaulu wao na kuweza kuwa kwenye kumi bora za shule bora hapa nchini naahidi kulivalia njuga suala hilo ilikuweza kufikia malengo”alisisitiza Dc Makota.

Kwa Upande wake mkurugenzi wa wilaya Kondoa Vijijini Falessy Kibassa alisema kuwa atahakikisha suala hilo linafanikiwa, lengo likiwa kuwawezesha waalimu na wadau kufikia malengo tarajiwa ya ufaulu na atalivalia njuga katika kuhakikisha masuala ya elimu wilayani humo yanakuwa ya mafanikio na mfano wa kuigwa mkoani hapa.

Nae Afisa elimu msingi Alphonce Mwamwile alisema kuwa sekta ya elimu wilayani humo japokuwa inakabiliwa na changamoto kubwa za uhaba wa waalimu katika shule nyingi pamoja na utoro, ukosefu wa chakula mashuleni wakati wa mchana watajitahidi kuhakikisha elimu inakuwa sanjari na ufaulu wa wanafunzi.

Afisa elimu Sekondari Hildacard Saganda alisema kuwa kumekuwepo na changamoto kubwa ya umaliziaji wa maabara katika shule za sekondari hivyo kuwakosesha wanafunzi wanaojifunza masomo ya sayansi kukosa kujifunza kwa vitendo ila watahakikisha wanashirikiana na wadau wengine katika kutatua changamoto hiyo.

Kwa upande mwingine Mbunge wa Kondoa vijijini Ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Ashatul Kijaji ameahidi kutoa Photocopy mashine kwa ajili ya mitihani ya kila mwezi kwa wanafunzi wa shule za wilaya hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...