Picha ya pamoja ya wadau wa elimu Tanzania na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Bunge, huduma na Maendeleo ya Jamii baada ya kikao cha kuwasilisha mapendekezo ya wadau wa elimu katika bajeti ya elimu ya mwaka wa fedha 2017/2018 uliofanyika katika ukumbi mdogo wa bunge mjini Dodoma.

Baada ya Kikao hicho wanakamati ya bunge ya kudumu huduma na maendeleo ya jamii waliahidi kuyafanyia kazi mapendekezo yaliyotolewa na wadau wa elimu ili kuboresha kiwango cha elimu hapa nchini Tanzania.
Makamu Mwenyekiti wa kamati ya bunge ya kudumu huduma na maendeleo ya jamii, Mhe. Azzan Zungu akifungua kikao na kuwakaribisha wadau wa elimu waliofika katika mkutano huo ili kuwasilisha mapendekezo na maoni kuhusu bajeti ya elimu ya mwaka 2017/18.
Kiongozi wa wadau wa elimu Tanzania(Head of Deligation) , Ndugu Saddam Khalfan akielezea madhumini ya kikao hicho kilichokuwa kinahusiha kuwasilisha mapendekezo na maoniya wadau wa elimu katika bajeti ya elimu ya mwaka 2017/18 kilichofanyika katika ukumbi mdogo wa Bunge mjini Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...