Teddy na Talkia Tumbi ambao ni mtu na dada yake wamefanya uzinduzi wa studio ya nywele na kuuza shanga na vito (jewelry) iliyopo kwenye mji wa Clemmons, North Carolina nchini Marekani. Studio hiyo ambayo ilizinduliwa siku ya Jumamosi May 13, 2017 ilihudhuriwa na Watanzania mbalimbali waliofika kuwaunga mkono.
Teddy Tumbi akimwandalia mteja (hayupo pichani)shanga alizonunua kwenye studio yao iliyofunguliwa siku ya Jumamosi May 13, 2017 Clemmons, North Carolina nchini Marekani. Studio hii ya kutengeneza nywele na kuuza shanga na vito (Jewelry) na anuani kamili ni 2575 Old Glory Road, Clemmons, NC 27012 simu 336 343 8170.

Wapili kushoto ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Watanzania North Carolina, Bi. Glory Alex akipata matunda ya ufunguzi wa studio hiyo kwa kutengeneza nywele zake alipokwenda kuwaunga mkono Teddy na Talkia Tumbi mtu na dada yake walipofungua studio ya nywele na kuuza shanga na vito.

Mmoja ya wateja akitengeneza urembo wa nywele studioni hapo.
 
Muonekano wa studio.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...