Ditha nyoni - RUVUMA

Raia nane kutoka nchi ya Ethiopia wamekutwa wamefariki katika kijiji cha Amani makolo taarafa ya kingonsera wilayani mbinga mkoani wa ruvuma huku wengine 25 wakiwa hai wanashikiriwa na jeshi la polisi.

Habari kutoka jeshi la polisi mkoa wa ruvuma kupitia kaimu kamanda wa polisi ACP DISAMASI KISUSI zinasema raia hao wa Ethiopia walikuwa wanasafirishwa kwenda nchi ya AFRIKA KUSINI kupitia Upande wa MALAWI mwa ziwa NYASA.

Vifo vya Waithiopia hao vinatokana na kubebwa kwenye kontena la lori wakitokea NAMANGA, ARUSHWA hivyo kutokana na hali mbaya ya hewa hali zao zilianza kubadilika na kupelekea kufariki.huku miili ya marehemu hao ikiwa imehifadhiwa katika hospitali ya wilaya MBINGA
Jeshi la polis mkoa wa ruvuma kwa kushirikiana na jeshi la uhamiaji linaendelea na uchunguzi kubaini walioleta miili ya marehemu na wale wasiliokamatwa hatua za kisheria zitafuatwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...