Baadhi ya wafanyakazi wa kitengo cha Corporate Support cha NMB wakipiga
picha na mmoja wa wanufaika wa wanufaika wa upasuaji wa mdomo Sungura
uliotolewa na wafanyakazi wa kitengo cha Corporate Support cha Benki ya
NMB.
WAFANYAKAZI
wa Benki ya NMB katika kitengo cha Corporate Support wamedhamini
upasuaji wa watoto wanne wenye midomo Sungura waliokuwa wamelezwa katika
hospitali ya CCBRT jijini Dar es Salaam. Akizungumzia udhamini huo,
Meneja Mwandamizi wa Idara ya Usimamizi wa Majengo NMB, Elizabeth Lukaza
alisema ufadhili huo ni sehemu ya utaratibu ambao wamejiwekea wao kama
wafanyakazi wa kitengo cha Corporate Support kusaidia jamii kwa sehemu
yenye uhitaji.
Alisema
ufadhili huo ulikuwa wa Dola 1,200 (Tsh. 2.6 milioni) na hiyo siyo mara
ya kwanza wao kutoa ufadhili kwa kuchangia huduma mbalimbali za kijamii
kwani kila mwaka hufanya hivyo angalau mara tatu.
“Kila
mwaka tunatoa msaada kwa jamii, kwa mwaka huu tumekuja CCBRT tumesaidia
watoto wanne ambao walikuwa wanatakiwa kufanyiwa upasuaji wa mdomo
Sungura, upasuaji wa kila mtoto tumetao Dolla 300," “Pesa hizi
tumejichangisha katika kitengo na ofisi imetuchangia sehemu ya fedha ili
kufanikisha lengo letu, tumekuwa tukifanya mambo mbalimbali, tumewahi
hata kutoa damu kwenye kituo chao kilichopo Mwananyamala,” alisema
Elizabeth.
Mmoja wa wanufaika wa ufadhili wa wafanyakazi wa kitengo cha Corporate
Support cha NMB, Emmanuel Isdor (mtoto), akiwa amebebwa na mama na
mamae, Maines Ephrahim.[/caption] Pia alizungumzia mipango ya kitengo
chao kwa siku zijazo, “Kuna vitu vingi vya kufanya, kama kitengo chetu
tumemua kuunga mkono juhudi za benki kupitia kitengo cha masuala ya
uwajikikaji kwa jamii (CSR).
Pia
tutaendelea kufuatilia maendeleo ya afya za watoto hawa kupitia wazazi
wao,” Naye mmoja wa wazazi ambao mtoto wake amefanyiwa upasuaji wa mdomo
Sungura kwa ufadhili wa NMB kupitia kitengo cha Corporate Support,
Maines Ephrahim alionyesha Furaha na kuwashukuru NMB kwa ufadhili huo na
kueleza kuwa kabla ya upasuaji huo hali ya mtoto ilikuwa tofauti na
ilivyo sasa.
“Nawashukuru
NMB kwa msaada ambao wamempatia mtoto wangu (Emmanuel Isdor),
amefanyiwa upasuaji vizuri…kabla ya upasuaji mtoto alikuwa analialia,
lakini sasa hali ni nzuri nimefurahi,” alisema Maines. Kwa upande wa
nesi aliyewahudumia katika wodi ya watoto wenye mdomo sungura na
walemavu, Joyce Cosmas alisema, “Nawashukuru NMB kwa msaada waliotoa,
kwa sisi kama manesi tuliwapokea vizuri na kuwapa huduma zote ambazo
walikuwa walistahili kuzipata.”
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...