Meneja Masoko na Mawasiliano wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF, James Mlowe, akitoa ufafanuzi mbele ya Wahariri wa vyombo vya habari,kuhusiana na namna mfuko huo unavyoweza kuhudumia wateja wake,katika semina iliyofanyika leo mapema leo jijini Dar.Pichani kati ni
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Theophil Makunga pamoja na Katibu wa Jukwaa hilo Neville Meena. 
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Theophil Makunga akichokoza Mada zilizowasilishwa na wataalamu wa mfuko huo wa LAPF,mbele ya Wahariri wa Vyombo vya Habari,zikiwemo mada zilizohusu Afya,mambo ya Uzazi kwa akina mama,Mafao mbalimbali ikiwemo fao la Elimu,fao la Kujitoa.Pichani kulia ni Meneja Masoko na Mawasiliano wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF, James Mlowe,kushoto ni Ofisa Mwandamizi Mipango na Uwekezaji, Eliya Shola pamoja na Meneja Mafao wa LAPF, Ramadhan Mkeyenge kutoka LAPF
Mmoja wa Wahariri akiuliza swali kuhusiana na huduma mbalimbali zitolewazo na mfuko huo wa LAPF.
Meneja Mafao wa LAPF, Ramadhan Mkeyenge, akitoa mada katika semina hiyo.Mkeyenge alisema kuwa mfuko huo mpaka sasa umeweza kutoa mafao na mikopo kama vile,mafao ya uzazi ambapo zimetolewa zaidi ya bilioni 12,mkopo wa elimu zaidi ya bilioni moja zimetolewa,mkopo wa kujikimu zaidi ya bilioni 5,mikopo ya nyumba zaidi ya bilioni 2,pamoja na hayo akaongeza kusema kuwa pia kuna waliolipwa kabla ya muda wa kustaafu Zaidi ya bilioni moja.
Ofisa Mwandamizi Mipango na Uwekezaji, Eliya Shola, akitoa ufafanuzi kuhusiana na uwekezaji mbalimbali unaofanywa na mfuko huo,ikiwemo katika suala la viwanda na namna ambavyo imechukua tahadhari katika suala zima la usimamizi wa viwanda hivyo
Ofisa Habari wa Mfuko wa LAPF, Rehema Mkamba (kushoto), akiwa na baadhi ya wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa kwenye semina hiyo.


Wahariri wa Vyombo vya habari wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikijadiliwa kwenye Semina hiyo ilioandaliwa na LAPF,na kufanyika mapema leo jijini Dar.Picha na Michuzi JR.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...