Na Karama Kenyunko, Blogu ya jamii.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewafutia kesi washtakiwa watatu waliokuwa wanakabiliwa na kesi ya dawa za kulevya zenye thamani ya zaidi ya milioni 25 na kuamuru wasikamatwe.

Amesema washtakiwa hao wasikamatwe na kushtakiwa kwa kufunguliwa shtaka linalofanana na hilo labda kwa maelekezo ya Mahakama Kuu.

Hatua hiyo ua kufuta kesi hiyo imekuja baada ya washtakiwa kuwa rumande kwa zaidi ya miaka mitatu bila ya upelelezi kukamilika na jalada ya polisi kutokuwepo mahakamani mara kadhaa. Washtakiwa walioachiwa huru ni, Salma Juma , Amos Sosoma na Rashid Mtitu.

Kesi hiyo iliyokuwa na namba 21 ya mwaka jana imefutwa na Hakimu Mkazi Mkuu, Respicius Mwijage baada ya kukaa mahakamani hapo kwa miaka mine bila ya upelelezi kukamilika.

Amesema Machi 6, mwaka huu, mahakama iliamuru upande wa mashtaka ifikapo Machi 23, itoe taarifa juu ya hatua ya upelelezi lakini ilipofika siku hiyo upande wa mashtaka ulidai upelelezi bado haujakamilika na jalada la polisi halipo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...