Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Watu wawili wanashikiliwa kwa tuhuma za kukutwa na nyara za serikali za Meno ya Tembo vipande sita ambavyo vilivyokamatwa Chanika jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi (CP), Somon Sirro amesema kuwa  vipande hivyo vilikamatwa wakati polisi wakifanya operesheni kupata taarifa ya watu wanataka kufanyabiashara ya kuuza vipande sita vya meno ya tembo na kwenda kuwatia hatiani nje ya nyumba ya moja ya watuhumiwa hao.

Watuhumiwa hao ni Mfanyabiashara Senei Abbas (36) pamoja na  Juma Mkong’wa (33) Fundi Ujenzi Mkazi wa Gongolamboto  jijini Dar es Salaam.
Wakati huo huo Jeshi la Polisi linamshikilia Mwanafunzi wa Chuo cha St. Joseph, Lewis Mbise (23) kwa tuhuma za kukutwa na silaha aina ya Luger CZ yenye namba za usajili C 4122 ikiwa na risasi 13 ndani ya magazine .

Mwanafunzi huyo alipohojiwa alivyopata silaha na kukiri kuwa aliiba kwa baba yake pamoja na fedha Tasilimu sh.800,000.
Jeshi polisi limeagiza kukamatwa kwa baba wa manafunzi kwa kukosa kutunza silaha mpaka mwanae anapata nafasi ya kwenda kuiiba.
Katika hatua nyingine Jeshi la Polisi inawashilikilia watu watatu kwa tuhuma za kuvujisha mtihani wa kidato cha Sita ambao unafanyika hivi sasa.

Watuhumiwa hao ni Mwalimu  Mussa Elius , Mwalimu Innocent Mrutu pamoja na mwanafunzi wa Kidato  cha Sita, Ritha Mosha .
Kamanda Sirro amesema wanaaendelea na mahojiano kuhusiana na mtihani  wa kidato cha sita unaoendelea kufanyika.

Jeshi la Polisi linawashikilia watuhumiwa watatu ambao ni walinzi kituo cha Mafuta cha Camel Kurasini kwa kula njama za wizi wa mauta lita 36000 zenye thamani ya sh. Milioni 72.

Walinzi hao Hamis Peter (49) mkazi wa Charambe, Jumanne Hamis (35) pamoja na Huruka Ramadhan (37).
 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) ofisini kwake jijini Dar es Salaam  leo. Picha na Emmanuel Massaka, Globu ya Jamii.
 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro akionyesha vipande vya meno ya tembo vilivyokamtwa na jeshi hilo leo jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro akionyesha silaha waliokamata kwa mwanafunzi ambayo aliiba kwa baba yake  leo jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...