WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Mkutano Mkuu wa Wadau wa Tasnia ya Korosho utakaofanyika kwa siku mbili kuanzia Jumamosi, Mei 13, 2007, mjini Dodoma.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho (CBT) Hassan Jarufu, amesema ya kuwa Mkutano huo Mkuu wa Wadau wa Tasnia ya Korosho utawajumuisha washiriki wapatao 600 na utafanyika kwenye Ukumbi wa Chuo cha Mipango, Dodoma.

“Kama tulivyokwishakueleza, Mkutano huu Mkuu utafunguliwa na Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa na watakuwapo pia Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Dk. Charles Tizeba, Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa inayolima Korosho ya Lindi, Pwani, Tanga, Mtwara na Ruvuma.

“Tumealika pia waheshimiwa Wabunge wanaotoka katika Mikoa hiyo, wakulima wa Korosho na watendaji wa Vyama vya Ushirika vya zao la Korosho. Mkutano huu utajadili kwa kina changamoto zinazoikabili Tasnia ya Korosho nchini,” alisema Jarufu.

Mkutano huu Mkuu wa Wadau wa Tasniaya Korosho unakuja katika wakati ambao Tasnia ya Korosho imepata mafanikio muhimu katika msimu uliopita ambayo ni pamoja na kuweka udhibiti uliosababisha Korosho nyingi kuuzwa kwa kutumia mfumo wa Stakabadhi Ghalani na hivyo kupunguza matumizi ya Kangomba, kipimo ambacho kwa muda mrefu kimekuwa kikimnyonya mkulima.

Udhibiti huo ulisababisha makusanyo ya Korosho kuongezeka kutoka tani 155, 244.645 msimu wa 2015/2016 hadi tani 264, 887. 527 katika msimu wa 2016/2017.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...