Waziri wa Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mh. Mwigulu Lameck Nchemba
wa pili kushoto akitoa Maelekezo kwa
Watendaji Wakuu wa Wizara yake
wakati wa Kikao cha cha maandalizi ya mwisho cha kupitia Bajeti ya Taasisi ziliko katika Wizara yake, kabla
ya kuiwasilisha Bajeti ya Wizara yake katika Vikao vya Bunge la Bajeti la Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania siku ya Jumanne. Kushoto kwake ni Naibu Waziri wa
Wizara hiyo Mhandisi Hamadi Masauni na wa kwanza kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali
Projest Rwegasira, Kikao hicho kimefanyika leo katika ukumbi wa Mikutano
wa Wizara mjini Dodoma.
Mkuu wa Jeshi la Polisi
nchini (IGP) Ernest Mangu aliyenyanyua mkono akitoa ufafanuzi wa jambo fulani
kuhusu bajeti ya Jeshi la Polisi nchini
mbele ya Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Lameck
Nchemba wakati wa Kikao cha Mapitio ya
Bajeti ya Taasisi ziliko katika Wizara
hiyo, ikiwa ni maandalizi ya mwisho kabla ya Bajeti ya Wizara hiyo
kuwasilishwa kwenye Vikao vya Bunge la
Bajeti la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,siku ya jumanne.Kikao hicho kilichowashirikisha
Watendaji Wakuu wa Wizara hiyo na Maafisa Mipango wa Wizara kimefanyika leo
katika ukumbi wa Mikutano wa wizara hiyo
mjini Dodoma.
Waziri wa Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mwigulu Lameck Nchemba
akipokea taarifa mbalimbali zilizotolewa na watendaji wakuu wa Wizara
yake wakati wa Kikao cha Maandalizi ya mwisho ya kupitia ya Bajeti ya Taasisi ziliko katika Wizara yake, kabla ya kusomwa kwa Bajeti ya Wizara yake
katika Vikao vya Bunge la Bajeti la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania siku ya
Jumanne. Kushoto kwake ni Naibu Waziri
wa Wizara hiyo Mhandisi Hamadi Masauni, Kikao hicho kimefanyika leo katika
ukumbi wa Mikutano wa wizara mjini
Dodoma.
Kamishna Jenerali wa Jeshi
la Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa wa
pili kulia akitoa ufafanuzi mbele ya Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,
Mwigulu Lameck Nchemba wakati wa Kikao
cha Mapitio ya Bajeti ya Taasisi ziliko
katika Wizara hiyo, ikiwa ni
maandalizi ya mwisho kabla ya Bajeti ya
Wizara hiyo kuwasilishwa kwenye Vikao
vya Bunge la Bajeti la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,siku ya Jumanne.Kikao
hicho kilichowashirikisha Watendaji Wakuu wa Wizara hiyo na Maafisa Mipango wa
Wizara kimefanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo mjini Dodoma.
Kamishna Jenerali wa Jeshi
la Zimamoto na Uokoaji nchini, Thobias Andengenye wa tatu kulia akitoa ufafanuzi kuhusu Jeshi lake mbele ya Waziri
wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Lameck Nchemba wakati wa Kikao cha maandalizi ya mwisho ya
kupitia ya Bajeti ya Taasisi ziliko
katika Wizara hiyo, kabla ya Bajeti ya
Wizara hiyo kusomwa kwenye Vikao vya Bunge la Bajeti la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania,siku ya Jumanne.Kikao hicho kilichowashirikisha Watendaji Wakuu wa
Wizara hiyo na Maafisa Mipango wa Wizara kimefanyika leo katika ukumbi wa
Mikutano wa Wizara hiyo mjini Dodoma.
PICHA
ZOTE NA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...