Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Mwigulu Lameck Nchemba  wa pili kushoto akitoa Maelekezo kwa  Watendaji Wakuu wa  Wizara yake wakati wa Kikao cha cha maandalizi ya mwisho cha kupitia Bajeti  ya Taasisi ziliko katika Wizara yake, kabla ya kuiwasilisha Bajeti ya Wizara yake katika Vikao vya Bunge la Bajeti la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania siku ya Jumanne. Kushoto kwake ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhandisi Hamadi Masauni na wa kwanza kulia ni  Katibu Mkuu wa Wizara  ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira, Kikao hicho kimefanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa  Wizara mjini Dodoma. 
 Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Ernest Mangu aliyenyanyua mkono akitoa ufafanuzi wa jambo fulani kuhusu bajeti  ya Jeshi la Polisi nchini mbele ya Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Lameck Nchemba  wakati wa Kikao cha Mapitio ya Bajeti  ya Taasisi ziliko katika Wizara hiyo,  ikiwa ni maandalizi  ya mwisho kabla ya Bajeti ya Wizara hiyo kuwasilishwa kwenye  Vikao vya Bunge la Bajeti la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,siku ya  jumanne.Kikao hicho kilichowashirikisha Watendaji Wakuu wa Wizara hiyo na Maafisa Mipango wa Wizara kimefanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa  wizara hiyo mjini Dodoma. 
 Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Lameck Nchemba  akipokea taarifa mbalimbali zilizotolewa na watendaji wakuu wa Wizara yake wakati wa Kikao cha Maandalizi ya mwisho ya kupitia ya Bajeti  ya Taasisi ziliko katika Wizara yake,  kabla ya kusomwa kwa Bajeti ya Wizara yake katika Vikao vya Bunge la Bajeti la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania siku ya Jumanne. Kushoto kwake ni  Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhandisi Hamadi Masauni, Kikao hicho kimefanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa  wizara mjini Dodoma. 
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza  nchini, Dkt. Juma Malewa wa pili kulia akitoa ufafanuzi mbele ya Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Lameck Nchemba  wakati wa Kikao cha Mapitio ya Bajeti  ya Taasisi ziliko katika Wizara hiyo,  ikiwa ni maandalizi  ya mwisho kabla ya Bajeti ya Wizara hiyo kuwasilishwa kwenye  Vikao vya Bunge la Bajeti la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,siku ya Jumanne.Kikao hicho kilichowashirikisha Watendaji Wakuu wa Wizara hiyo na Maafisa Mipango wa Wizara kimefanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa  Wizara hiyo mjini Dodoma. 
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini, Thobias Andengenye wa tatu kulia  akitoa ufafanuzi kuhusu Jeshi lake mbele ya Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Lameck Nchemba  wakati wa Kikao cha maandalizi ya mwisho ya kupitia ya Bajeti  ya Taasisi ziliko katika Wizara hiyo,  kabla ya Bajeti ya Wizara hiyo kusomwa kwenye Vikao vya Bunge la Bajeti la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,siku ya Jumanne.Kikao hicho kilichowashirikisha Watendaji Wakuu wa Wizara hiyo na Maafisa Mipango wa Wizara kimefanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa  Wizara hiyo mjini Dodoma. 
PICHA ZOTE NA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...