DROO
ya 13 ya Biko waendeshaji wa mchezo wa kubahatisha Tanzania maarufu
kama ‘Ijue Nguvu ya Buku’, imefanyika leo asubuhi, huku mkazi wa Mbezi jijini
Dar es Salaa, Amani Kabuku, mwenye miaka 23, akifanikiwa kuibuka na
ushindi mnono wa Sh milioni 20.
Mshindi
huyo ameibuka katika droo iliyochezeshwa jana jijini Dar es Salaam na
Balozi wa Biko, Kajala Masanja, kwa kushirikiana na mwakilishi wa Bodi
ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Abdallah Hemed.
Akizungumza
katika droo hiyo leo asubuhi, Meneja wa Huduma kwa Wateja wa Biko, Grace Kaijage,
alisema ni wakati wa kutajirika kwa kupitia mchezo wao wa Biko uliozidi
kujizolea umaarufu katika kipindi kifupi tangu kuanzishwa kwake nchini
Tanzania.
Alisema
anaamini washindi wao wanaoendelea kujipatia fedha mbalimbali kupitia
mchezo wao, huku akiwataka Watanzania waendelee kucheza kwa kufanya
miamala ya fedha kwenye simu zao za Tigo Pesa, M-Pesa na Airtel Money
kwa kuanzia Sh 1,000, ambapo namna ya kucheza ni kuweka namba ya kampuni
ambayo ni 505050 na ile ya kumbukumbu 2456.
“Wanachotakiwa
kufanya ni kucheza mara nyingi zaidi ili wajiwekee mazingira mazuri
yaushindi wa zawadi mbalimbali kuanzia Sh 5,000, 10,000, 20,000, 50,000,
100,000, 500,000 na Sh Milioni moja, huku zikilipwa moja kwa moja
kupitia simu zao za mikononi walizotumia kuchezea Biko,” Alisema Grace.
Balozi
wa Biko Tanzania, Kajala Masanja kulia akiwa kwenye majukumu ya
kumtafuta mshindi wa droo ya 13 ya Biko ambapo kijana mwenye miaka 23
mkazi wa Mbezi Makonde, jijini Dar es Salaam, Amani Kabuku, alifanikiwa
kuibuka na zawadi nono ya Sh Milioni 20. Kushoto ni mwakilishi wa Bodi
ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Abdallah Hemed.
Kajala
Masanja kulia akizungumza huku akionyesha namba ya mshindi wa Sh
Milioni 20 kutoka Mbezi Makonde, jijini Dar es Salaam baada ya
kutangazwa mshindi katika droo iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam,
huku akishuhudiwa na mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha
Tanzania, Abdallah Hemed.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...