Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
Aliyekuwa mshambuliaji wa timu ya Toto Afrika Waziri Junior ametambulishwa leo mbele ya waandishi wa habari baana ya kusaini kandarasi na timu ya Azam.
Azam jana walifanikiwa kupata saini ya mshambuliaji huyo kinda kutoka Toto ikiwa ni katika muendelezo wa kuboresha kikosi chao ili kuweza kufanya vizuri katika msimu ujao unaokuja.
Akizungumza na waandishi wa habari, Afisa habari wa Azam Jafar Iddy amesema kuwa wamefanikiwa kunasa saini ya mshambuliaji juyo kinda kutoka Toto kwani hilo limekuja ikiwa ni moja ya mapendekezo ya kocha mkuu wa timu hiyo.
"huu ni muendelezo wa kusajili na kufa nya marekebisho katika kikosi chetu kuelekea msimu ujhao, na usajili huu unakuja baada ya kuona mapendekezo ya kocha mkuu Aristoc Cioaba na akwa sasa ni kuwapa fursa vijana,"amesema Iddy
Awali Waziri alikuwa anawaniwa na timu Yanga lakini Azam wameonekana kuwapiga bao na kumsainisha kwa dau nono .
Afisa habari wa Azam Jafar Iddy(wa pili kulia) akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kumtambulisha mshambuliaji yao mpya Waziri Junior (wa pili kushoto) aliyesaini kandarasi ya kuitumikia klabu hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...