Na Zainab Nyamka-Globu ya Jamii.

TIMU ya Mtibwa Sugar imewatema wachezaji saba wakikosi hicho waliomaliza mikataba yao na kufanikiwa kusajili chipukizi wawili wapya ambao ni beki wa kati, Hussein Iddi na mshambuliaji Salum Ramadhani kw ajili ya msimu mpya wa mwaka 2017/18. 

Katika wachezaaji saba walioruhusiwa kuondoka katika timu hiyo ni pamoja na aliyewahi kuwa mshambuliaji wa Yanga Said Bahanuzi baada kumaliza mkataba wake 

Mkurugenzi wa Mtibwa Sugar, Jamal Bayser amesema kuwa beki Hussein Idd ametokea katika timu ya JKT Oljoro ya Arusha na Salum Ramadhani ametokea Polisi Morogoro na kila mmoja amesaini mkataba wa miaka miwili kila mmoja na ni matumaini ya Mtibwa Sugar watang’ara Manungu. 

Pamoja na hayo, Bayser amesema kwamba wanatarajia benchi la Ufundi chini ya Kocha Mkuu Zubeiry Katwila kupandisha baadhi ya wachezaji kutoka katika timu ya vijana ya Mtibwa Sugar. 

“Uongozi wa Mtibwa Sugar unaendelea kufanyia kazi mapendekezo ya benchi la ufundi, hivyo basi usajili bado unaendelea na nyota wengine wanatarajiwa kuingia makubaliano na Mtibwa Sugar wakati wowote kuanzia sasa,”amesema. 

Aidha, Bayser amesema kwamba Mtibwa Sugar imeachana na Jaffary Salum Kibaya, Said Mkopi, Maulid Gole ‘Adebayor’, Said Bahanuzi, Vincent Barnabas, Ally Lundenga na Ally Shomary ambao wamemaliza mikataba yao. 

Mtibwa inasifika mno kwa kuibua wachezaji chipukizi kutoka timu mbalimbali ndogo na wengine kupandisha kutoka kikosi chake cha vijana ambao baadaye hugeuka lulu na kugombewa na timu kubwa, hususan Simba na Yanga.
Said Bahanuzi akimtoka kwa kasi beki mwingine wa JKT

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...