Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), pamoja na Naibu wake Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), pamoja na Naibu Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Mhe. Mhandisi Stella Manyanya (Mb), wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Chuo cha Ualimu Bustani kilichoko wilayani Kondoa mkoani Dodoma, walipotembelea bungeni mjini Dodoma, siku ambayo Bunge limepitisha kwa kishindo Bajeti ya Sh. trilioni 31.7 kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) akimshukuru na kumpongeza Naibu wake Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), kwa ushirikiano mkubwa aliompatia hadi kufanikisha kazi kubwa ya kuandaa na kusimamia Bajeti Kuu ya Serikali ya shilingi trilioni 31.7 iliyopitishwa na Bunge kwa kishindo mjini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kushoto), akiteta jambo na maafisa waandamizi wa Wizara yake nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma, baada ya Bunge kupitisha kwa kishindo Bajeti Kuu ya Serikali ya shilingi trilioni 31.7

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...