Picha na Habari za Freddy Macha
Baadhi yetu
huwaita wenye hali hii “taahira” – neno la asili ya Kiarabu lenye maana “mtu asiye sawa” (wazimu, chizi,
bwege, nk). Sahihi ni “mtindio ubongo” –
kwa Kiingereza “Down Syndrome”....
Baadhi ya taswira zake ni : kufikiri na kuzungumza taratibu,
kigugumizi, mwili mfupi, utofauti wa tambo la kichwa,vidole vya mikono
na miguu,nk.
Mbali na kuwanyanyapaa, jamii zetu Afrika bado hazitambui umuhimu wa kuendeleza
wenye ulemavu.
Mwaka huu kijana wa miaka 18, Samwel Mwanyika, mwenye “Mtindio
Ubongo “ (Down Syndrome) alikuwa mshindi
wa kimataifa wa upigaji picha.
Balozi wetu Uingereza Mheshimiwa Asha-RoseMigiro
akaeleza:
“Wametoka vijana wengi kwenye nchi zilizoendelea, wengine wamemzidi umri...tena
wenzetu huwa na mipango maalum ya kuwapa mbinu mbalimbali,...sasa huyu wa
familia ya kawaida tu ya Kitanzania ambapo bado hatujaweka miundo mbinu kama
walivyoweka huku, picha yake
imeshinda...”
Mwasisi wa kujitolea
wa shirika la Mtindio Ubongo (Pearl of People with Down Syndrome) , Mony
Teri Pettite na wazazi wake Samwel,
Philip Mwanyika na Sophie Mshangama, walikutana na Balozi Migiro na kupongezwa Ijumaa iliyopita. Afisa
Utawala Ubalozini, Rose Kitandula , pia alikuwepo.
Picha ya Samwel Mwanyika iliyonyakua tuzo la kimataifa la Stephen Thomas, mjini London.
Samwel Mwanyika na picha iliyonyakua tuzo la kimataifa la Stephen Thomas, mjini London.
Balozi Migiro akimvika Samwel Mwanyika bendera ya taifa,
alipowakaribisha na familia ofisini kwake, Ijumaa 16, Juni 2017.
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...