Na Bashir Nkoromo
Hatimaye
Mjumbe wa kamati Kuu ya CCM, Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi na Mbunge
wa Kuteulia na Rais Alhaj Abdallah Bulembo, amemaliza ziara yake ya
Kichama akiwa amefanikiwa kutembelea mikoa saba na jumla ya Wilaya 47 za
mikoa hiyo.
Katika
ziara hiyo ambayo alianza May 26, 2017, aliihitimisha jana, Juni 10,
2017 katika mkoa wa Geita, ziara ikiwa imechukua zaidi ya wiki mbili,
ambapo mkoa wa kwanza kufanya ziara hizo uliuwa Dar es Salam na badaye
kuendelea katika mikoa ya Dodoma, Manyara, Tabora, Kigoma, Kagera na
Geita ambao ndio mkoa aliomalizia.
Alhaj
Bulembo katika ziara hiyo ambayo haikuhusu Jumuia yake ya Wazazi
Tanzania, bali ya Kichama zaidi ilikuwa mahsusi kwa kuagizwa na Bosi
wake, Mwenyekiti wa CCM Rais John Magufuli, kwa lengo la kutoa shukrani
kwa wana CCM kufuatia kura nyingi walizompa hadi kukipatia Chama Cha
Mapinduzi kura nyingi wakati wa Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 2015.
Hata
hivyo Bulembo anasema, Shukrani hizo, ni za awali kwa kuwa Mwenyekiti
Mwenyewe Rais Dk. John Magufuli atafanya ziara rasmi kutoa shukrani.
Mjumbe
wa kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akisiriki kuapa wakati
wanachama wapya waliohamia CCM kutoka Chadema walipokuwa wakiapa na
kuungwa mkono na wanachama wote katika kiapo hicho
Wanachama wapya wa CCM wakiapa
Wanachama wa CCM wapya wakiapa huku wakiungwa mkono na wanachama wote waliokuwa ukumbini, kula kiapo hicho
Alhaj Bulembo akimvalisha kofia mmoja wa wanachama hao wapya
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...