DAU nono la
Sh Milioni 10 linalotolewa kama zawadi ya droo kubwa ya Mchezo wa Kubahatisha
wa Biko limeenda kwa Junior Ashery Pesambili wa Lupela, Makete, mkoani Njombe,
ikiwa ni mwendelezo wa kugawa fedha kwa washindi wake ikitokana na matokeo ya droo
ya 11 iliyochezeshwa jana Jumapili.
Droo hiyo
iliyochezeshwa jana iliendeshwa na Balozi wa Biko Kajala Masanja, akishirikiana
na mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Bakari Maggid. Akizungumza
katika droo hiyo jana, Meneja wa Huduma kwa Wateja wa Biko, Grace Kaijage,
alisema wamedhamiria kugawa mamilioni kwa washindi wao wanaocheza mchezo wa
Biko uliozidi kushika kasi katika kona mbalimbali nchini Tanzania.
Alisema
tayari wameshafanya droo 11 kubwa ambapo watu mbalimbali wameendelea kupokea
fedha zao ikihusisha vijana bila kusahau mzee Stanley Kapondo naye aliyekuwa
miongoni mwa Watanzania waliovuna zawadi mbalimbali kutoka Biko.
“Kucheza
Biko mara nyingi zaidi ndio nafasi kubwa ya kuibuka na ushindi, hivyo ni wakati
wa Watanzania kucheza mara nyingi ili washinde, ukizingatia kuwa mbali na donge
nono la Milioni 10 linalotolewa Jumatano na Jumapili, pia mtu anaweza kushinda
zawadi mbalimbali kuanzia Sh 5,000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000,
1,000,000, huku droo ya Jumatano hii ikitoa Sh Milioni 20 kwa mshindi wake kama
ilivyokuwa Jumatano iliyopita.
“Mchezo wetu
unachezwa kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi kwa kufanya miamala kwenye simu
za Tigo Pesa, M-Pesa na Airtel Money ambapo utakapoingia kwenye kipengele cha
Lipa Bili au lipa kwa Mpesa, mshiriki wetu ataingiza namba ya kampuni 505050 na
baadaye kuweka namba ya kumbukumbu 2456, huku akianzia kucheza kwa Sh 1000 au
zaidi,” Alisema Grace.
Balozi
wa Biko Tanzania, Kajala Masanja, kulia akionyesha namba ya ushindi wa
Sh Milioni ya mshindi wao wa Lupela, Makete,mkoani Njombe, Junior Ashery
Pesambili aliyepatikana katika droo ya jana Jumapili. Kushoto ni
mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Bakari Maggid.
Balozi
wa Biko Kajala Masanja akifurahia namba ya mshindi wa Sh Milioni 10
kutoka Makete, mkoani Njombe, droo iliyochezeshwa jana jijini Dar es
Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...