Na Mwamvua Mwinyi, Bagamoyo
RAIS
mstaafu wa awamu ya Nne ambae pia ni mkulima wa tunda la mnanasi
,dk.Jakaya Kikwete,amewataka wamiliki wa viwanda vya matunda kuacha
kuwakandamiza wakulima kwa kununua matunda kwa gharama ya chini .
Amesema
viwanda hivyo vinasaidia kupatikana kwa masoko ya ndani lakini vimekuwa
havina uwiano wa gharama zinazolingana na maumivu anayoyapata
mkulima.Aidha dk. Kikwete ameeleza kumekuwa na changamoto ya kushuka kwa
soko kwa wakati mwingine hali inayokuwa ikisababisha wakulima kupata
hasara kwa matunda kuoza yakiwa mashambani .
Akitoa
taarifa ya shamba lake la mananasi lililipo Bago-Kiwangwa wilayani
Bagamoyo ,wakati Mwenge wa Uhuru ulipokwenda kutembelea shamba hilo
,alisema kilimo cha matunda kina tija endapo utalima kisasa na kuwa na
soko la uhakika .
Kikwete
alieleza ,viwanda vya usindikaji matunda mbalimbali ,vinapaswa kumjali
mkulima ambae amekuwa akipata shida na kutumia gharama kubwa kuandaa
shamba .“Wakati utafika watakosa matunda ,kutokana na gharama yao
hailipi ,wakulima wa matunda tushindwa kukubali kuuza kwa bei ya chini
ambayo hailipi ” alifafanua .
Rais mstaafu wa awamu ya nne dk .Jakaya Kikwete akishika Mwenge wa Uhuru uliopita kutembelea shamba lake la mananasi lililopo Bago -Kiwangwa Bagamoyo .(Picha na Mwamvua Mwiny.
Rais mstaafu wa awamu ya nne dk .Jakaya Kikwete na mkewe mama Salma Kikwete wakikimbiza Mwenge wa Uhuru uliopita kutembelea shamba lake la mananasi lililopo Bago -Kiwangwa Bagamoyo .
Kongozi wa mbio za mwenge kitaifa Amor Hamad ,akizungumza baada ya kupata taarifa ya ujenzi ,wa kiwanda cha kusindika matunda cha sayona kilichopo Mboga – Msoga Chalinze ,kutoka kwa afisa uhusiano wa kampuni mama ya MMI ,Abubakar Mlawa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...