Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi ametoa rai kwa vyuo vikuu na vyuo vinavyotoa elimu ya juu kuwa sehemu ya kuwafundisha na kuwatengeneza wasomi wenye kutambua fursa na tija za maisha na sio sehemu ya kuendekeza migomo isiyo na faida katika maisha ya wanachuo hao.

Dkt. Nchimbi ametoa rai hiyo jana wakati akizindua kikundi cha Bright Focus kilichopo chuo cha Uhasibu tawi la Singida chenye wana kikundi 89 ambao ni wanachuo, walimu na walezi wenye malengo ya kutambua fursa za kuboresha maisha.

Amesema wakati akizindua kikundi hicho anatambua kuwa kikundi hicho kitasaidia kubuni mawazo yenye tija, fursa, na mwelekeo wa kuboresha uchumi huku akiwasisitiza kuelekezana namna bora ya matumizi ya rasilimali walizonazo hususani rasilimali fedha.

Dkt Nchimbi amekitaka kikundi hicho kuwa chachu ya mabadiliko ya tabia na mienendo yote mibaya iwe mizuri kutokana na baadhi ya wanachuo katika vyuo mbalimbali kuhusishwa na tabia zisizo njema.

Amesema kila mwanakikundi anapaswa anatakiwa mawazo yake yaendane na malengo ya kikundi cha Bright Focus kuanzia mwenendo wa maisha yake, ufaulu wake na hata matumizi ya rasilimali yawe yenye muono wa kutengeneza faida na hasa kujifunza namna ya kuhifadhi akiba.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi (katikati) akipiga ngoma kwa furaha kama ishara ya kuzindua kikundi cha Bright Focus kilichopo chuo cha Uhasibu Singida, kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Singida Elias Tarimo.
1
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akihutubia wanakikundi cha Bright Focus (hawapo pichani) kikundi hicho kipo chuo cha Uhasibu Singida.
2
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi (katikati) akipiga ngoma kama ishara ya kuzindua kikundi cha Bright Focus kilichopo chuo cha Uhasibu Singida, kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Singida Elias Tarimo.
3
Wanachuo ambao ni wanakikundi cha Bright Focus kilichopo Chuo cha Uhasibu Singida wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Singida wakati wa uzinduzi wa kikundi hicho.
4
Makamu wa rais wa Bright Focus John Gama akiwasilisha malengo ya kikundi hicho kwa Mkuu wa Mkoa wa Singida wakati wa uzinduzi katika chuo cha Uhasibu Singida.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...