Na Ripota wa Globu ya Jamii

Zaidi ya wasanii kumi na mbili wa timu ya bongo fleva kusakata kabumbu na wadau wao wakubwa wa redio E-fm siku ya Jumamosi tarehe 25/06/2017 katika uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza katika mwendelezo wa kutambulisha masafa mapya ya EFM Radio ya 91.3 fm Mwanza.

Kwa mujibu wa taharifa iliyotlewa na afisa uhisiano wa kituo hicho, Jesca Mwanyika amesema kuwa wakali hao wa bongo fleva na Efm redio watashiriki katika mtanange huo ili kuipa jamii hamasa katika kujikita kwenye michezo mbalimbali ili kuimarisha afya zao na kuepuka hatari ya kupata magojwa yasioambukizwa.

“ mechi hii ni sehemu ya utaratibu wa E-fm ya kuwafikia wadau wao kama ilivyoada yao, vilevile kutoa wito kwa makampuni mbalimbali kuwekeza katika michezo ili kuhamasisha na kuvumbua vipaji vipya katika jamii” amesema Mwanyika .

Mechi hiyo itaenda sambamba na mazoezi ya mbio za mwendo pole (jogging) zikiongozwa na Efm jogging club, Kubandika stika vyombo vya moto, na kuweka kifaa cha kuongeza masafa katika redio za daladala kwa madereva hamsini wa kwanza kufika uwanjani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...