Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

MABINGWA Ligi Kuu Tanzania Bara Vodacom (VPL) Yanga leo wameaga amashindano ya SportPesa Super Cup kwa mikwaju ya penati 4-2 katika mchezo wa hatua ya nusu fainali yanayoendelea kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Mechi hiyo iliyochezwa katika uwanja wa Uhuru ulianza majira ya saa 8 kamili kwa kuzikutanisha timu ya Yanga dhidi ya AFC Leopard ya nchini Kenya.Mpaka dakika 90 za mpira zinamalizika timu hizo zilitoshana nguvu kwa kutoka suluhu na kuelekea kwenye mikwaju ya penati.

Timu zote zilionekana kushambulia kwa kupokezana lakini safu za ushambiaji hazikuwa makini na kupoteza nafasi walizozipata mara kadhaa.

Yanga walifanya mabadiliko kwa kumtoa Emanuel Martin na kuingia Said Musa, akatoka Maka Edward na kuingia Said Makapu, Yusuph Mhilu alitoka na kuingia Samwel Greyson na Pato Ngonyani alitoka na kuingia Babu Ally.
AFC Leopard wakafanya mabadiliko kwa kumtoa Abwao Marcus na kuingia Ingotsi Marselas.

Wachezaji waliopiga penati kwa upande wa Yanga ni Nadir Haroub, Obrey Chirwa ambao walipata na Said Makapu na Said Musa kukosa kwa upande wa Yanga.Kwa upande wa AFC Leopard ni golikipa Jan Otieno, Otieno Duncan, Bernad Mango na Katerega Allan ambao walipata na Ingotsi Marselas alikosa.
Beki wa Yanga, Juma Abdul, (kulia) akiruka kuwania mpira na beki wa AFC Leopards Abwao Marcus, wakati wa mchezo Nusu Fainali wa mashindano ya SportPesa Super Cup, uliochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, leo. Katika mchezo huo AFC Leopards wameibuka na uwashinda wa mikwaju ya penati 4-2 baada ya kumalizika dakika 90 kwa sare ya 0-0.
Mshambuliaji wa Yanga Juma Mahadhi (kulia) akiwania mpira na Kiungo wa AFC Leopards, Alan Katerega, wakati wa mchezo Nusu Fainali wa mashindano ya SportPesa Super Cup, uliochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Mshambuliaji wa Yanga Juma Mahadhi (kulia) akimtoka mpira na beki wa AFC Leopards, Abdallah Salim, wakati wa mchezo Nusu Fainali wa mashindano ya SportPesa Super Cup, uliochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. 

Mshambuliaji wa Yanga Obrey Chirwa, akijiandaa kupiga shuti huku akizongwa na mabeki wa AFC Leopards, wakati wa mchezo Nusu Fainali wa mashindano ya SportPesa Super Cup, uliochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...