Wafanyakazi wa Manispaa ya Ilala pamoja na wafanyakazi wa Green Waste Pro Ltd wakiendelea kufanya usafi katika fukwe ya Bahari ya Hindi kata ya Kivukoni eneo la Aga Khan jijini Dar ikiwa ni wiki ya Mazingira. Mwenye shati nyeupe ni Meneja Msaidizi wa kampuni Green WastePro ltd, Erick Mark.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema akisitiza jambo kwa wadau walioshiriki zoezi la usafi katika fukwe ya bahari ya Hindi eneo la Aga Khan na kuwaomba waendelee na kufanya usafi na hata kuwahamasisha watu wengine kuwa mabalozi wa mazingira ili kufikia malengo waliyojiwekea katika manispaa ya Ilala.
Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala , Mstahiki Omary Kumbilamoto akizungumza jambo kwa wadau mbalimbali waliokuja kujumuika katika zoezi la usafi katika fukwe ya Bahari ya Hindi eneo la Agha Khan katika wiki ya mazingira.
Meneja wa uendeshaji wa kampuni ya Green Waste ProLtd, Abdallah Mbena akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ushiriki wa kampuni hiyo katika zoezi la kufanya usafi katika fukwe ya Bahari ya Hindi kata ya Kivukoni eneo la Aga Khan jijini Dar ikiwa ni wiki ya Mazingira.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Green WastePro Ltd mara baada ya kumaliza kufanya usafi kwenye fukwe ya Bahari ya Hindi eneo la Aga Khan kata ya Kivukoni ikiwa ni maadhimisho ya wiki ya Mazingira.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...