Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni,Hashim Mgandilwaakimshukuru Bw. Hamodu H. Mvungi mara baada ya kushiriki katika futari hiyo pamoja na wageni mbalimbali waliohudhuria.
Bw. Hamidu H. Mvungi miliki wa kijiji cha Hamidu City Park, Mikwambe Kibada Kigamboni chenye nyumba 1500 akizungumza na wageni waalikwa mbalimbali waliohudhuria katika futari aliyowaandalia wageni wake wakiongozwa na Mkuu wa wilaya ya Kigamboni Mh .Hashim Mgandilwa ambapo aliwashukuru wageni waalikwa hao kwa kujumuika naye katika futari hiyo katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhan, huku akiwatambulisha makazi hayo yenye nyumba za kuuza ambapo ameshirikiana na mabenki mbalimbali na kukopesha kwa watu wanaohitaji nyumba katika kijiji hicho.
Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni,Hashim Mgandilwa na Mwenyeji wake Bw. Hamidu Mvungi wakiongoza wageni waalikwa katika futari hiyo.
Baadhi ya wageni waalikwa mbalimbali waliohudhuria katika futari hiyo wakichukua chakula.
Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni,Hashim Mgandilwa katikati , Mwenyeji wake Bw. Hamidu Mvungi pamoja na wageni wake wakipata futari.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Kigamboni, Rahel Mhando pamoja na wageni mbalimbali waalikwa wakishiriki katika futari hiyo iliyoandaliwa na Bw. Hamidu Mvungi nyumbano kwake Kigamboni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...