Na Karama Kenyunko

⁠⁠⁠⁠⁠UPANDE wa mashtaka katika kesi ya dawa za kulevya inayomkabili msanii wa filamu Wema Sepetu na mwenzake umebadilisha hati ya mashtaka dhidi ya washtakiwa.

Hatua hiyo imekuja leo baada ya wakili wa Serikali Constatine Kakolaki kuomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuomba kufanya mabadiliko hati ya mashtaka kabla ya kuwasomea maelezo ya awali.

Mapema Mwezi uliopita mahakama hiyo iliambiwa kuwa upelelezi wa kesi umekamilika na Leo ilikuwa inakuja kwa ajili ya kuwasomea washtakiwa maelezo ya awali (PH).

Wema na wafanyakazi wake Angelina Msigwa na Matrida Abas wamesomewa mashtaka mapya mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba ambaye alikubaliana na ombi la upande wa mashtaka.

Katika mashtaka hayo mapya, washtakiwa wanakabiliwa na mashitaka mawili la kukutwa na kiwango kidogo cha dawa za kulevya na kutumia dawa za kulevya.

Akiwasomea mashyaka hayo amedai, February 4, mwaka huu katika makazi yao Kunduchi Ununio, washtakiwa walitenda kowa.Imedaiwa kuw siku hiyo washtakiwa wote walikutwa na msokoto mmoja na vipisi vya bangi vyenye uzito wa gramu 1.08.

Aidha katika shtaka la pili linalomkabili Wema peke yake imedaiwa kuwa kati ya Februari Mosi na 3, mwaka huu, jijini Dar es Salaam, Wema alitumia dawa za kulevya aina ya bangi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...