‘SHIRAWADU’ ni ngoma mpya kabisa ya mduara ambayo wiki hii imeachiwa rasmi kutoka kwa msanii anayekuja juu kwa kasi ya ajabu, Shania Kabeya.
Studio ya 442 Music iliyoko Karakata, Kipawa, jijini Dar es Salaam chini ya Mtayarishaji Tamimu Hamis ‘Mabanga’ ndipo ilipopikwa ngoma hiyo iliyobeba ujumbe mzito juu ya wapenzi wanavyotakiwa kutoyafuatilia maneno ya watu wa pembeni.
Kwa upande wake Shania mwenyewe, hii ndio ngoma yake ya kwanza ambapo hata hivyo yuko mbioni kuandaa kazi nyingine ‘sumu’, anazoamini kuwa zitabamba zaidi na kutokea kufunika nyingine zitakazozikuta.
Video ya kibao ‘Shirawadu’ iko jikoni na itatoka mwishoni mwa mwezi huu, ikiwa sambamba na kibao chake kingine kipya cha mduara. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...