‘SHIRAWADU’ ni ngoma mpya
kabisa ya mduara ambayo wiki hii imeachiwa rasmi kutoka kwa msanii anayekuja
juu kwa kasi ya ajabu, Shania Kabeya.
Studio ya 442 Music iliyoko
Karakata, Kipawa, jijini Dar es Salaam chini ya Mtayarishaji Tamimu Hamis
‘Mabanga’ ndipo ilipopikwa ngoma hiyo iliyobeba ujumbe mzito juu ya wapenzi
wanavyotakiwa kutoyafuatilia maneno ya watu wa pembeni.
Kwa upande wake Shania
mwenyewe, hii ndio ngoma yake ya kwanza ambapo hata hivyo yuko mbioni kuandaa
kazi nyingine ‘sumu’, anazoamini kuwa zitabamba zaidi na kutokea kufunika
nyingine zitakazozikuta.
Video ya kibao ‘Shirawadu’ iko
jikoni na itatoka mwishoni mwa mwezi huu, ikiwa sambamba na kibao chake kingine
kipya cha mduara.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...