Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
KAMPUNI ya Bima ya Jubilee Insurance imezindua kampeni ya ISHI HURU kwa watoto wa darasa la tatu lililoanza Juni 12 na litamalizika rasmi tarehe 30 Juni mwaka huu ikizihusisha shule zote za Serikali.
Katika shindano hili, mwanafunzi wa darasa la tatu atatakiwa kuchora picha zinazoelezea na kuonesha mtazamo wake kuhusu nini maana ya neno ‘ishi huru’ (live free).
Akizungumza kwa niaba ya kampuni ya Bima ya Jubilee, Mhasibu Mkuu Hellena Mzena amesema kuwa Jubilee imeandaa shindano liitwalo  hilo la ‘Ishi Huru’  ambalo washiriki watakuwa ni wanafunzi wa darasa la tatu wa shule zote za msingi za serikali.
Hellena amesema washindi wa Tano watakaopatikana watazawadiwa Bima ya Elimu yaani “Jubilee Career Life Cover” watakayoipata watakapojiunga na elimu ya sekondari na kila shule itakayotoa mshindi itapata zawadi ya kikombe na cheti cha kutambua ushindi huo.
Mgeni Rasmi Kamishna wa Mamlaka ya usimamizi wa Bima Tanzania , Dr. Baghayo Saqware akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa kampuni ya Bima ya Jubilee baada ya kuzindua kampeni ya 'Ishi Huru' itakayomalizika Juni 30 mwaka huu pamoja na Mkuu wa Shule ya Madenge Lissy Kaluvya, Diwani na Naibu Meya wa Temeke Feisal ....
Mgeni Rasmi Kamishna wa Mamlaka ya usimamizi wa Bima Tanzania , Dr. Baghayo Saqware pamoha na Mkuu wa Shule ya Madenge Lissy Kaluvya wakizindua shindano la 'Ishi Huru' uliofanyika katika shule hiyo leo Jijini Dar es salaam.
Mkurugezi wa Bodi ya Wakurugenzi ya Jubilee Life Insurance; Mr. Karim Jamal akizungumza na kuwashukuru Shule ya ,Msingi ya Madenge kwa kuweza kukubali kukarabati shule yao.
Mhasibu Mkuu kampuni ya Bima ya Jubilee Hellena Mzena akisoma risala kwa Mgeni rasmi kuhusiana na kampuni yao ya Jubilee pamoja na jitihada wanazozifanya katika kuhakikisha wanasaidia jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...