WAKATI
leo ni siku ya unywaji maziwa duniani kampuni ya maziwa ya Asas
Dairies Limited imenywesha maziwa wanafunzi zaidi ya 4000 wa shule
mbali mbali za Manispaa ya Iringa .
Shule hizo za msingi zilizopo kanda ya Ruaha ambazo zimeanza kunufaika na unywaji maziwa ,huku walimu wao wakidai baadhi ya wanafunzi wa shule hizo wamekuwa na matokeo mabaya katika mitihani kutokana na unywaji wa pombe ya kienyeji aina ya ulanzi .
Shule hizo za msingi zilizopo kanda ya Ruaha ambazo zimeanza kunufaika na unywaji maziwa ,huku walimu wao wakidai baadhi ya wanafunzi wa shule hizo wamekuwa na matokeo mabaya katika mitihani kutokana na unywaji wa pombe ya kienyeji aina ya ulanzi .
Meneja wa miradi wa kampuni ya Asas Dairies Ltd Hassan Swedi alisema kuwa maadhimisha ya mwaka huu yamelenga zaidi vijana hasa wanafunzi wa shule za msingi mjini Iringa na ndio sababu kampuni yake imelazimika kutoa msaada wa maziwa na majaketi kwa wanafunzi wanaotoka katika familia duni .
Alisema kuwa kampuni hiyo inaamini kuwa iwapo shule zitaweka utaratibu wa kutoa maziwa kwa wanafunzi afya za wanafunzi hao zitakuwa bora na kiwango cha elimu kinaweza kuongezeka zaidi mashuleni.
Mbali ya unywaji wa maziwa kuhamasishwa zaidi mashuleni bado viongozi wa serikali wanapaswa kuanza kuhamasha unywaji wa maziwa katika ofisi hizo za umma badala ya kutumia maziwa kutoka nje ya nchi .
Alisema kuwa kampuni ya Asas Dairies
Ltd imeendelea kuunga mkono mpango wa lishe mashuleni kama njia ya kuboresha afya na uwezo wa wanafunzi kufanya vizuri kwenye masomo Iringa unazalisha maziwa zaidi ya lita milioni 14 kwa mwaka ila bado kiwanda cha Asas kinasindika lita 400,000 pekee kwa siku .
Meneja miradi wa kampuni ya maziwa ya Asas Dairies Ltd Hassan Swedi akimpa maziwa mlemavu
leo siku ya unywaji maziwa duniani
wafanyakazi wa kampuni ya Asas wakigawa maziwa kwa wanafunzi leo siku ya unywaji maziwa duniani .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...