Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Kanali Mstaafu Ngemela Lubinga akimkaribisha Ofisini kwake, Mwenyekiti wa CCM Tawi la Uingereza (UK), Kangoma Kapinga, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, leo. Mwenyekiti huyo ambaye alifuatana na Katibu wa CCM wa tawi hilo Leybab Mdegela alifanya mazungumzo na Kanali Lubinga ikiwemo haja ya kuimarishwa matawi ya CCM yaliyopo nchi za nje.
Mwenyekiti wa CCM Tawi la Uingereza Kangoma Kapinga akisaini kitabu cha wageni Ofisini kwa Kanali Ngemela (katikati), kabla ya mazungumzo yao kuanza. Kushoto ni Katibu wa CCM Tawi la Uingereza Leybab Mdegela.
Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Kanali Mstaafu Ngemela Lubinga akifafanua jambo wakati akizungumza na Mwenyekiti wa CCM Tawi la Uingereza Kangoma Kapinga (kulia), katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, leo. Kushoto ni Katibu wa CCM wa tawi hilo Laybab Mdegela. PICHA: BASHIR NKOROMO-CCM Blog.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...