Kanda ya kati (Dodoma) imekusanya kiasi
cha Tshs. 1,426,273,033.70 ya Makusanyo
ya Kodi ya Pango la Ardhi, sawa na 204% ya
malengo na hivyo kuvuka malengo iliyopangiwa. Kamishna Msaidizi wa Ardhi, kanda
ya kati Dodoma; Hezekiel Kitillya ameeleza wakati akizungumza na Waandishi wa Habari.
Kamishna Kitillya alisema; tathimini iliyofanyika
ni ya mpaka 31 Mei, 2017. Malengo ya Makusanyo yaliyokuwa yamepangwa na Wizara ya
Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/17
- 30 Juni, 2017 yalikuwa ni kukusanya kodi ya Tshs. Bilioni
111.77, ambapo kati ya kanda nane za
ardhi zilizopo nchini, kanda ya kati ilipangiwa kukusanyaTshs. Milioni 700.
Vile vile, baadhi ya Halmashauri tayari zimeshavuka malengo
ya makusanyo zilizowekewa, kama vile Manispaa ya Dodoma, malengo yalikuwa Tshs. 200,000,000/= na makusanyo
yakawa; Tshs.678,804,841.40, Manispaa ya
Singida, malengo yalikuwa Tshs. 200,000,000/= na makusanyo yakawa
Tshs.308,392,069.17 na Halmashauri ya Manyoni, malengo yalikuwaTshs.
100,000,000/= na makusanyo yakawa Tshs. 117,200,000.00. Pia Halmashauri nyingine
za Wilaya ya Itigi, Chamwino, Bahi; nazo zimeshavuka malengo na nyingine zilizobaki
zikikaribia kufikia malengo.
Akieleza moja ya mkakati muhimu ambao umewezesha
kanda yake kuvuka malengo ni pamoja na kusambaza hati za madai Demand notes. Alisema; “Halmashauri zote
zilielekezwa kuandaa na kusambaza hati za madai kwa wadaiwa wakubwa sugu”.
Akizungumzia moja ya changamoto Kuu inayokabili
zoezi la Makusanyo; Alisema ni Wananchi kutokuwa na uelewa wa kutosha kuhusu tofauti
ya Kodi ya Pango la Ardhi na Kodi ya Majengo, ambapo Wananchi wengi hudhani wakishajenga
nyumba na kuanza kulipa kodi ya jengo, hawapaswi tena kulipa kodi ya pango la
Ardhi.
Aidha, Kamishna Kitillya ametoa wito kwa
Wananchi kuhamasika kulipa Kodi ya Pango la Ardhi kwa mujibu wa Sheria na kwa Maendeleo
ya Taifa. Aliongeza kuwa; “Sasa Kodi ya Pango
la Ardhi imeboreshwa kwa kumuwezesha mwananchi kutambua kiasi anachodaiwa na kufanya
malipo hayo kieletroniki, kwa kutumia Tovuti ya Wizara au simu kwa tigo pesa au
m-pesa, tofauti na ilivyokuwa awali ambapo Mwananchi alilazimika kufika katika vituo
vya malipo, katika Halmashauri yake”.
Kanda
yakati (Dodoma) inahudumia mikoa miwili (2) Dodoma na Singida yenye jumla ya Halmashauri
kuminatano (15).
Kamishna
wa Ardhi msaidizi – Kanda ya Kati (Dodoma); Hezekiel Kitillya akizungumza
na A Fm Radio - 92.9 – Dodoma; kuhusu Tathimini ya Malipo ya Kodi ya Pango
la Ardhi ya Kanda na Maboresho ya ulipaji wa Kodi hiyo kwa njia ya
Kielektroniki.
Mwananchi
akifurahia kupata elimu na kupatiwa kipeperushi kwa elimu zaidi kuhusu Kodi ya
pango la Ardhi katika mojawapo ya Saloon za kusuka, mjini Dodoma.
Vipeperushi
vya kuelimisha jamii kuhusu Kodi ya
Pango la Ardhi vikigaiwa kwa Wananchi katika Stand ya Mabasi mjini Dodoma
Vipeperushi vya kuelimisha jamii kuhusu Kodi ya Pango la Ardhi vikigaiwa kwa Wananchi katika Stand ya Mabasi mjini Dodoma
Kamishna
wa Ardhi msaidizi – Kanda ya Kati (Dodoma); Hezekiel Kitillya akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu Utekelezaji wa
Majukumu ya Ofisi yake, Tathimini ya Malipo ya Kodi ya Pango la Ardhi ya Kanda
na Maboresho ya ulipaji wa Kodi hiyo kwa njia ya Kielektroniki. Kushoto kwake
ni Mwanasheria na Afisa Ardhi mwandamizi; Jane Kapongo na kulia kwake ni
Msajili wa Hati katika kanda hiyo; Geoffrey Mauya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...