Usafi wa kila mwisho wa mwezi waimarisha mazingira nchini

KILA ifikapo Juni 5 kila mwaka, zaidi ya nchi 100 zinaadhimisha Siku ya Mazingira Duniani. Jovina Bujulu wa Idara ya Habari (MAELEZO) anaelezea umuhimu wa siku hii ambayo hapa nchini itaadhimishwa tarehe 3 na 4 mkoani Mara katika kijiji cha Butiama. 

Madhumuni makubwa ya maadhimisho haya ni kuhamasisha jamii duniani kote kuelewa masuala yanayohusu mazingira na pia kuhamasisha watu kulinda na kuhifadhi mazingira. Aidha, ni siku ambayo jamii inatakiwa kutambua umuhimu wa kulinda na kuhifaddhi mazingira kwa ustawi na maendeleo ya nchi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Rais, Muungano na Mazingira, maadhimisho hayo mwaka huu yatafanyika kijijini Butiama ili kumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na kukumbuka mchango wake mkubwa katika masuala ya mazingira.

Wakati wa maadhimsho hayo shughuli mbalimbali zitafanyika zikiwemo kupanda miti, kuendesha mijadala mbalimbali na kongamano la viongozi kuhusu mazingira na pia kufanya maonyesho ya shughuli za mazingira.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo ambayo Kauli Mbiu ya mwaka huu niHifadhi ya Mazingira: Muhimili kwa Tanzania ya Viwanda atakuwa Makamu wa Rais, Mh. Samia Suluhu Hassan. Kaulimbiu hii inahamasisha Utunzaji wa mazingira wakati tukielekea uchumi wa viwanda.

Tarehe 9 Desemba mwaka jana, Rais wa Awamu ya Tano Dkt. John Pombe Magufuli aliamuru kusitisha maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Uhuru wa Tanganyika na badala yake siku hiyo iadhimishwe kwa kufanya usafi wa mazingira nchini kote. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Tunaishukuru sana serikali ya awamu ya tano kwa kutoa tamko la kusitisha matumizi ya mifuko ya plastiki nchini.Ni wakati muafaka sasa kusubiri kanuni husika ili sheria ichukue mkondo wake kwa wale watakaokaidi agizo hili lililosubiriwa kwa muda mrefu sana na wadau wa mazingira nchini.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...