Askari
wa Usalama Barabarani akichukua maelezo ya gari Noah yenye namba za
usajili T338 BVU iliopata ajali mapema jana,njia panda Goba,Mbezi Beach
jijini Dar.Baadhi ya Mashuhuda wa tukio hilo walieleza kuwa chanzo cha
ajali hiyo ni mwendo kasi wa gari dogo (daladala pichani chini yenye
namba za usajili T912 CVY),iliyokuwa imebeba abiria ikitokea Goba kwenda
Mwenge,na hivyo gari hiyo kukosa mwelekeo kufuatia kona kali iliyopo eneo
hilo,Katika ajali hiyo hakuna aliyepoteza maisha.
Mashuhuda
hao pia wakatoa wito kwa baadhi ya Madereva kuwa makini,kufuata sheria
na kuzingatia alama za barabarani,kwani kwa kufanya hivyo ajali nyingi
zitapungua kutokea.
Daladala yenye namba za usajili T912 CVY ikiwa imeacha barabara na
kuvamia mtaro kufuatia gari hiyo kupoteza uelekeo kwa kile lichodaiwa na
Mashuhuda kuwa ni mwendo kasi na kutaka kugongana uso kwa uso na gari
nyingine aina ya Noah (pichani juu),sehemu yenye kona kali.
Baadhi
ya watu wakishuhudia ajali ya gari aina daladala pichani yenye namba
za usajili T912 CVY,ikiwa imeacha njia na kuvamia mtaro,kama ionekavyo
pichani.katika ajali hiyo hakuna aliyepoteza Maisha
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...