Na. Immaculate Makilika- MAELEZO 

Februari 2015,  Rais wa Jamhuri ya Kenya Uhuru Kenyatta alimkabidhi Rais mstaafu wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete nafasi ya Uenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika mkutano wa 16 wa Wakuu wa Jumuiya hiyo Jijini Nairobi Kenya. 

Kutokana na hali ya mgogoro wa kisiasa katika nchi ya Burundi, ambayo ilipaswa kukabidhiwa nafasi ya Uenyekiti wa Jumuiya mwaka 2016, Wakuu wa  Jumuiya hiyo waliamua kwa kauli moja kuwa Tanzania kupitia Rais Dkt. Rais John Pombe Magufuli kuendelea na nafasi hiyo. 

Katika Mkutano wa 18 wa kawaida wa Wakuu wa Jumuiya hiyo uliofanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 20 Mei,2017,  Rais Magufuli alisema katika kipindi cha  Uongozi wa Tanzania katika Jumuiya hiyo  mafanikio mbalimbali yalipatikana ikiwemo utekelezaji wa ajenda ya utengamano katika eneo la ushuru wa forodha linaloshuguhulikia vikwazo vya biashara visivyo na kodi. 

Anasema katika ushirikiano wa kifedha Tanzania imewezesha kuandwa miswada ya uanzishwaji wa taasisi ya fedha ya Jumuiya itakayokuwa Taasisi ya mpito kabla ya kuanzishwa kwa Benki kuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. 

Aidha, Rais Magufuli alisema mafanikio mengine ni pamoja na ujenzi wa miundombinu ikiwemo mradi wa ujenzi wa barabara ya Arusha - Holili - Taveta hadi Voi, na kukamilika kwa upembuzi wa mradi wa barabara ya Malindi- Lungalunga- Tanga – Bagamoyo. 
Aidha Rais Magufuli alisema pia barabara za Lusahunga- Lusumo- Kigali na Nyakanazi- Kasulu- Rumonge –Bujumbura ziko kwenye hatua mbalimbali za usanifu, ikiwa ni sambamba na ujenzi wa vituo vya ukaguzi mipakani, ambapo vituo 9 kati ya 15 tayari vimeanza kufanya kazi.   

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...