MJASIRIAMALI mwanamke mwenye umri wa miaka 26, Magreth Sinyangwa amekabidhiwa jumla ya Sh Milioni 20 za ushindi wa bahati nasibu ya Biko, aliyoupata katika droo kubwa iliyochezeshwa juzi Jumatano, jijini Dar es Salaam, huku akiwa mwanamke wa kwanza kuibuka na ushindi huo.

Sinyangwa amekabidhiwa fedha hizo Kilosa katika benki ya NMB, mkoani Morogoro na Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, ambaye pamoja na mambo mengine, alimpongeza mshindi huyo na kumtaka azitumie fedha zake kwa uangalifu pamoja na kuboresha maisha yake ya kila siku.

Akizungumza katika makabidhiano hayo, Heaven alisema ni wakati wa kutajirika kwa kutumia vyema bahati nasibu ya Biko, ‘Ijue Nguvu ya Buku’ iliyozidi kuchanja mbuga na kutoa mamilioni ya Sh kwa washindi wa droo kubwa zinazofanyika Jumatano na Jumapili, sanjari na zawadi za papo kwa hapo.


“Tunajivunia kumpata mshindi mwanamke ambaye leo (jana) tumemkabidhi zawadi yake ya Sh Milioni 20, tukiamini kuwa atazitumia vizuri katika kuhakikisha kwamba anakuza biashara zake, ukizingatia kuwa tayari yupo kwenye tasnia ya biashara kabla ya kupata donge nono la Biko.


“Kucheza ni rahisi kwa sababu Biko inachezwa kwenye simu za Tigo Pesa, M-Pesa na Airtel Money, ambapo mtu atafanya muamala kuanzia Sh 1,000 na kuendelea ambapo ataweka namba ya kampuni ambayo ni 505050 na ile ya kumbukumbu ni 2456, huku mbali na donge nono la Sh Milioni 20 linatoka kila Jumatano na Jumapili, pia zipo zawadi za papo hapo kuanzia Sh 5,000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni,” Alisema Heaven.
Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven kulia akiwa katika makabidhiano ya Sh Milioni 20 kwa mshindi wao wa Kilosa, mkoani Morogoro, Magreth Senyangwa aliyeibuka kidedea katika droo kubwa iliyofanyika Jumatano iliyopita. Kushoto ni mume wa Magreth, Bahati Ramadhani na mwingine ni Ofisa wa NMB Tawi la Kilosa, akiwa kwenye makabidhiano hayo.
Mshindi wa donge nono la Sh Milioni 20 kutoka Kilosa, mkoani Morogoro, Magreth Senyangwa akiwa ameshika fedha zake baada ya kukabidhiwa kutoka kwa waendeshaji wa bahati nasibu ya Biko.
Meneja Masoko wa Biko Goodhope Heaven kushoto akiwa ameshika hundi tayari kwa kumkabidhi mshindi wao wa Sh Milioni 20 wa Kilosa Morogoro, Magreth Senyangwa, wa pili kutoka kushoto akifuatiwa na mumewe Bahati Ramadhan pamoja na familia yao.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...