Na Mary Gwera, Mahakama, Iringa
Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa imefanikiwa kuondosha Mashauri/kesi kwa zaidi ya asilimia tisini (90) na kuifanya Mahakama hiyo kuendana na azma ya Mahakama ya Tanzania ya kutoa haki kwa wakati ili kuondokana na mlundikano wa mashauri katika Mahakama zake nchini.
Akizungumza ofisini kwake katika mahojiano maalum na Mwandishi wa taarifa hii aliyepo Kanda ya Iringa, mapema Juni 6, Hakimu Mkazi Mfawidhi, Mahakama ya Hakimu Mkazi-Iringa, Mhe. David Ngunyale alisema hali ya uondoshaji wa Mashauri katika Mkoa wa Iringa inaridhisha na kufafanua kuwa kwa upande wa Mahakama za Mwanzo ambazo jumla yake zipo 21, hakuna kesi inayozidi miezi sita (6) katika Mahakama hizo.
Akiongelea katika ngazi ya Mahakama za Wilaya, Mhe. Ngunyale alisema kuwa Mahakama hizo zina jumla ya kesi 12 za mlundikano (ambazo zimezidi umri ya miezi 12 Mahakamani), huku kesi 8 zikiwa ni za Jinai na nne (4) zikiwa ni kesi za Madai.
 Hakimu Mkazi Mfawidhi, Mahakama ya Hakimu Mkazi-Iringa, Mhe. David Ngunyale
 Mtendaji wa Mahakama-Kanda ya Iringa, Bw. Elvin Mwakajinga
 Afisa Tawala, Mahakama ya Hakimu Mkazi/Mkoa-Iringa, Bi. Dorice Kisanga akionesha maboksi ambapo mafaili ya kesi zilizomalizika yalipohifadhiwa, kwa urahisi wa rejea ya kumbukumbu za kesi za nyuma.
Muonekano wa jengo la Mahakama Kuu-Kanda ya Iringa, katika uwanja huu, yapo pia majengo ya Mahakama ya Wilaya na Mahakama ya Hakimu Mkazi-Iringa. Kwa habari zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...