Mchezo wa soka ni mchezo ambao ili ufanikiwe hauhitaji jitihada za mtu mmoja ila jitihada za timu nzima kuanzia wachezaji,viongozi na benchi la ufundi. Klabu ya Simba imeweza kutembea katika tafsiri hiyo ya mafanikio ya soka yanahitaji ushirikiano wa timu nzima ili kufikia malengo waliyojiwekea.

Ni kitu ambacho wapenzi na wadau wengi wa soka hawajafahamu dhana ya viraka vilivyopo katika mpira na mwisho vinaunda mpira mwenyewe. Viraka vya mpira ni sehemu ya kuelezea muunganiko unaohitajika katika watu ili kuleta mafanikio ya kitu kizima na pia utofauti wa rangi katika viraka huelezea timu mbili tofauti katika uwanja zinazocheza mchezo wenyewe.

Msimu wa 2016/2017 umekua bora sana kwa klabu ya simba na kufanya klabu imalize ligi nikiwa nafasi ya pili na kufanikiwa kubeba kombe la Azam Sport Federation Cup ( ASFC) msimu huu katika fainali Kali dhidi ya Mbao fc ya Mwanza.

Maandalizi ya klabu ya Simba waliyoyafanya ndiyo matunda ya walichokipata na kitawaletea mafanikio zaidi kama wakiendekea nacho kwa misimu mingine inayokuja.

Moja ya eneo ambalo klabu ya simba ilikua na changamoto na kujikuta wanashindwa kujishika vizuri ilikua katika eneo la benchi la ufundi,naweza kusema Benchi la simba limetibiwa ipasavyo.

Joseph Omog huyu mkameruni ni moja ya makocha wazuri na wenye kuamini katika nidhamu ya mchezaji mmoja na baadae nidhamu ya klabu kwa ujumla. Hakuna asiyefahamu mafanikio aliyoyapaya Omog akiwa na klabu Fc Leopard ya Congo Brazzaville alipoifikisha katika fainali ya kombe la shirikisho katika fainali waliyocheza dhidi ya Sc vita ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Omog alijitangaza katika mashindano ya afrika kama ilivyo kwa George Lwandamina wa yanga alivyojitangaza kupitia Mashindano ya ligi ya mabingwa. Kabla ya ujio wa Omog klabu ya simba ilikua klabu iliyokua ikicheza soka safi lisilo na faida kwao kutokana na upungufu wa nidhamu ya mchezo kupitia utimamu wa mwili na kuhimili mikiki mikiki ya ligi kwa dakika tisini za mchezo.

Na Honorius Mpangala.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...