Na
Bashir Yakub.
Wanaokopa hela kwenye
taasisi za fedha
wanatakiwa kujua haki
walizonazo. Haki kabla ya
kuchukua mkopo, haki wakati
wa kuchukua mkopo, haki
wakati wa kurejesha,
na haki baada
ya kurejesha au kushindwa
kurejesha. Hautakiwi
kusubiri taasisi iliyokukopa
iwe ndiyo ya kukueleze haki
ulizonazo bali watakiwa ujue haki
hizo kwa jitihada
zako.
Taasisi ya fedha
inaweza kukueleza baadhi
ya haki lakini
ni muhali kukueleza
haki ambazo wao
zinawabana. Watakueleza haki
ambazo hazina madhara
kwao. Basi yakupasa
ulijue hili.
Masuala ya kuweka
rehani ili upate
mkopo yanaongozwa na
sheria mbili. Sheria
namba 4 ya
mwaka 1999 Sheria
ya ardhi, pamoja
nayo Sheria namba
17 Sheria ya
rehani ya mwaka
2008. Humo zimo haki nyingi
za mtoa mkopo
wakadhalika mchukua mkopo.
Hata hivyo tutatizama
haki moja tu ya
notisi kabla ya
kuuzwa kwa nyumba/kiwanja cha
mkopaji.
1.KUSHINDWA KUREJESHA
MKOPO.
Kifungu cha 127 ( 1 ) cha
sheria ya ardhi
kinaeleza habari ya
kushindwa kurejesha mkopo. Kifungu kimeieleza
habari hii ikiwa
miongoni mwa mambo
ambayo yanachukuliwa kama ukiukwaji wa masharti
ya mkataba wa
mkopo. Mengine ambayo
yanachukuliwa kama ukiukwaji
wa masharti ya
mkopo ni kuweka
rehani mara zaidi
ya mmoja kwa
taasisi tofauti, kuuza,
kupangisha wakati kuna
rehani bila taarifa
au ridhaa kutoka kwa
mtoa mkopo n.k. Hata
hivyo haya na
mengine yatachukuliwa kama
kukiuka masharti ya
mkopo ikiwa yamekatazwa
katika mkataba wako
na taasisi ya
fedha.
Pia kwa mujibu
wa kifungu hicho
kushindwa kurejesha mkopo
kunajumuisha pesa kamili
uliyoikopa, riba, pamoja na
makato mengine ambayo
yanajenga sehemu ya
mkopo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...