Na Bashir
Yakub
Wapo wazazi wanaowakatalia wazazi
wenzao kuwaona watoto/mtoto
baada ya kuwa
wameachana. Wengine hawakuachana
bali hawakuwahi hata kuishi pamoja isipokuwa
walizaa tu lakini
yule mzazi anayeishi
na mtoto anamzuia
mzazi mwenzake kumuona
mtoto husika. Basi makala
haya yatatizama jambo
hili kwa sura
ya sheria zetu.
Uhalali wake na
uharamu wake, hatua unazoweza
kuchukua na mtazamo
wa jumla ikiwa jambo
hili ni haki
kisheria ama laah.
Sheria namba 21
ya mwaka 2009
Sheria ya Mtoto
ndiyo itakayotupatia majibu
ya suala hili
kwa ujumla wake.
1.KUMUONA MTOTO
HUMAANISHA NINI.
Unapotizama kwa
ujumla sheria ya
mtoto hasa vile
vifungu vinavyozungumzia habari
ya kumuona mtoto
utaona kuwa vinazungumzia kumuona
mtoto kwa maana
ya hatua ya
baba mzazi, mama
mzazi, au mlezi
mwenye mamlaka kutembelea
eneo alilohifadhiwa mtoto
kwa ajili ya
kuonana na mtoto
huyo.
Haijalishi
anaumwa au yu
mzima, yuko kituo
cha kulelea watoto au
nyumbani kwa mtu, na
hali nyingine au
mazingira yoyote atayokuwemo. Pia kumuona mtoto
si tu kumuonesha
mtu kuwa mtoto
ni yule halafu
basi. Bali kumuona mtoto
kunajumuisha kumuona na
kumgusa kimwili.
2. JE NI
MTOTO WA UMRI
GANI ANAYEONGELEWA HAPA.
Kifungu cha 4
cha Sheria ya mtoto kinajibu swali
hili. Kifungu kinasema
kuwa mtu mwenye
umri wa chini
ya miaka 18
ataitwa mtoto . Kwa
hiyo tunapoongelea kumuona
mtoto tunamaanisha mtu
ambaye umri wake
uko chini ya
miaka 18 yaani
kuanzia miaka 17
kushuka chini. Mwenye
miaka 18 kamili
si mtoto kwa
maana ya kifungu
hiki.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...