MAMLAKA ya Viwanja vya Ndege nchini (TAA) imeshiriki kufanya usafi katika maeneo yanayozunguka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku mazingira duniani.

Wafanyakazi wa mamlaka hiyo wameshiriki shughuli hizo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani, ambayo kitaifa inaadhimishwa kesho katika Wilaya ya Butiama, mkoani Mara.

Akizungumza leo wakati wa kufanya usafi huo, Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo, Salim Msangi amesema, ndege za abiria zimekuwa zikizalisha hewa ya ukaa kwa asilimia mbili duniani kote, hivyo ni muhimu kupanda miti maeneo ya viwanja vya ndege ili kutunza mazingira.

Amesema kila mwaka wamekuwa wakipanda miti katika maeneo ya viwanja vya ndege ili kufyonza hewa ya ukaa ambayo kwa kiasi kikubwa inachangia kuharibu mazingira na kuongeza joto.

"Lakini pia nimeagiza mameneja wote kuhakikisha wanapanda na nitakuwa natoa zawadi kila mwaka kwa meneja atakayeonekana kufanya vizuri," amesema Msangi.

Amesema utunzaji wa mazingira ni muhimu kwani binadamu wote na viumbe hai vingine vinahitaji mazingira na kwamba hata kaulimbiu ya kitaifa ya mwaka huu ya “Hifadhi mazingira, Muhimu kwa Tanzania ya Viwanda” haiwezekani kuwa na viwanda katika mazingira ambayo si salama.
 Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka Viwanja vya Ndege nchini (TAA), Salim Msangi wa (kwanza kushoto) akiongoza ufanyaji  katika maeneo yanayozunguka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere leo jijini Dar es Salaam.
 Wafanyakazi wa Mamlaka Viwanja vya Ndege nchini (TAA), wakiendelea na  usafi.
Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka Viwanja vya Ndege nchini (TAA),Salim Msangi akiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa Mamlaka hiyo leo jijini Dar es Salaam. Picha na Emmanuel Massaka, Globu ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...