Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni ,Benjamini Sitta akizungumza wakatiwa kikao cha baraza la Madiwani katika ukumbi wa Manispa ahiyo Magomeni jijini Dar es Salaam, juni 15, 2017.

Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Baraza la Madiwani la Manispaa ya Kinondoni limeagiza kuhakikisha fedha zote zilizopo katika akaunti za kata zaidi ya Bilioni 4.9 zifanyiwe utaratibu wa manunuzi ili ziweze kutekeleza miradi iliyokusudiwa katika kata hizo.

Maazimio hayo yamefikiwa katika baraza la Madiwani wa Manispaa hiyo lililongozwa na Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo, Benjamini Sitta .

Aidha baraza hilo pia limeridhia maombi ya kamati ya Fedha kwa kutaka kubuni vyanzo vipya vya fedha vitakavyosaidia Halmashauri hiyo kupata fedha zaidi licha ya baadhi ya vyanzo kuhamia serikali kuu. 

pia kikao hicho kilipitisha azimio la kumpongeza Rais John Pombe Magufuli kwa kitendo chake cha kizalendo cha kuhakikisha kuwa fedha za watanzania zilikuwa zinapotea kutokana na mchanga wa Madini uliokuwa ukisafirishwa nje kiholela unapangiwa utaratibu wa kunufaisha Serikali.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni ,Aron Kangurumjuli aakizungumza wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani.
Diwani wa Kata ya Magomeni, Julian Bujugo akichangaia katika Mkutano wa Baraza la Madiwani Kinondoni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...