HALMASHAURI ya Manispaa ya Ubungo jijini Dar es Salaam imetiliana saini ya mikataba 30 yenye thamani ya Sh. bilioni nne na Wakandarasi kutekeleza shughuli mbalimbali katika halmashauri hiyo.

Akizungumza wakati wa utilianaji saini hizo uliofanyika katika Ofisi za Halmashauri hiyo Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, John Kayombo alizitaja shughuli zitakazohusika katika mikataba hiyo kuwa ni pamoja na usafi, barabara  na miradi ya maji.

 Meya wa Ubungo, Boniface Jacob (katikati)na  Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, John Kayombo (wa kwanza kulia ) wakisani mkatamba na Mkurungenzi wa Kampuni ya Invostment , Rukia Punzi leo jijini Dar es Salaam.

 “Manispaa yetu ina miezi minane tu lakini tumefanikiwa kusaini mkataba 30 ya miradi mbalimbali, tunaposaini mikataba hii inaonesha wazi kuwa Manispaa yetu inakua.

“Ombi langu kwenu, nendeni mkatekeleze kile kilichopo kwenye mikataba na bahati nzuri siwafahamu sitaweza kusita kuchukua hatua kama Meya, nitasimamia sheria sitapindisha pale nitakapoona kazi imeenda ovyo sitakuwa tayari kufungwa pingu” amesema Kayombo.

Kayombo aliwataka wakandarasi hao kuhakikisha wanatekeleza miradi waliokubalia isiishie kusaini kisha wakapotelea mitini.

Naye  Meya wa Manispaa hiyo, Boniphace Jacob, aliwataka wakandarasi hao kuhakikisha wanatekeleza miradi hiyo katika kiwango walichokubaliana na kuwa atakayetekeleza kinyume atanyang’anywa na kupewa mtu mwingine fedha zitarudishwa .

“Ukipewa miezi miwili ikiisha kabidhi mradi, mkurugenzi ukikuta mtu anayefanya kazi ya usafi hajasafisha au  mtu yeyote atakayekiuka mkataba tusiwe na aibu ya kumwajibisha” amesema Jacob.
 Meya wa Ubungo,  Boniface Jacob (kushoto)  akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, katika hafla ya kusaini mikataba 30 yenye thamani ya Sh.bilioni Nne na wakandarasi kutekeleza shughuli mbalimbali katika Halmashauri hiyo. kulia ni Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, John Kayombo,
Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, John Kayombo akizungumza katika hafla ya kusani mikataba 30 yenye thamani ya Sh bilioni nne na wakandarasi kutekeleza shughuli mbalimbali katika halmashauri hiyo.
 Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, John Kayombo akibadilishana hati za makubalino na Mkurungenzi wa Kampuni ya Invostment Rukia Punzi leo jijini Dar es Salaam.,katikati ni Meya wa Ubungo Mh. Boniface Jacob.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...