Katibu wa taasisi ya vijana ya Tanzania Youth Icon (TAYI), Abdallah Ahmed Suleiman akimuonyesha Mratibu wa Umoja wa Mataifa (UN)nchini,  Alvaro Rodriguez (wakwanza kushoto),ramani ya mpango wa uboreshaji huduma ya maji katika jimbo la Kikwajuni.Mratibu huyo amefika jimboni hapo ikiwa ni juhudi za Mbunge wa Jimbo hilo,Mhandisi Hamad Masauni(watatu kushoto) katika juhudi zake za kutatua changamoto za  huduma ya maji kwa wananchi.
 Mkurugenzi Uzalishaji Maji wa Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA), Mhandisi Mohamed Elyas, akitoa maelezo ya Mradi wa Maji Kikwajuni kwa Mratibu wa Umoja wa Mataifa (UN) nchini, Alvaro Rodriguez alipotembelea mradi huo uliopo katika jimbo la Kikwajuni,Zanzibar.
 Mratibu wa Umoja wa Mataifa (UN)nchini,  Alvaro Rodrigues, akiangalia moja ya mabomba yanayotumika kusafirisha maji kwenda kwenye maeneo mbalimbali jimboni Kikwajuni ikiwa ni sehemu ya ushirikiano na Mbunge wa Jimbo hilo,Mhandisi Hamad Masauni katika kuhakikisha anamaliza tatizo la upungufu wa maji jimboni hapo.
Kwa habari zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...