Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii ,Kanda ya Kaskazini
MAZISHI
ya Mbunge mstaafu wa jmbo la Moshi mjini na Mwenyekiti wa Chadema mkoa
wa Kilimanjaro Philemon Ndesamburo Kiwelu (82) yanataraji kufanyika kwa
siku mbili mfululilizo huku watu zaidi ya laki 2 wakitaraji kushiriki
katika mazishi hayo.
Shughuli
nzima za mazisihi zinataraji kufanyika June 5 na sita katika uwanja wa
mashujaa mjini Moshi kabla ya kuhitimishwa siku ya Jumanne kwa ibada
itakayoanzia kanisani na kumalizikia nyumbani kwa marehemu.
Hatua
ya maziko ya Ndesamburo kufanyika kwa siku mbili inatokana na uwepo wa
idadi kubwa ya marafiki wa familia kushiriki katika maziko hayo ya
kihistoria yatakayotanguliwa na kutoa heshima za mwisho ,shughuli
zilizopangwa kufanyika katika uwanja wa mashujaa mjini Moshi.
Akizungumza
mara baada ya kumalizika kwa kikao kilichodumu kwa zaidi ya saa nne
,Msemaji wa Chadema katika maandalizi ya mazishi hayo Amani Golugwa
amesema uamuzi huo unatokana na kutoa nafasi kwa watu mbalimbali kutoa
heshima za mwisho kwa Ndesamburo.
“Tumekua
na kikao na wanafamilia viongozi wa chama na mashaurizano kuhusiana na
msiba huu ,tumekuwa na watoto wa marehemu ,walikuwepo wachungaji na
viongozi wa chama ,kimsini tumekubaliana mazishi ya mze wetu Ndesamburo
yatafanyika kwa siku mbili mfululizo”alisema Golugwa.
Kikao cha Wanafamilia,Viongozi wa siasa na Viongozi wa Dini kikifanyika nyumbani kwa marehemu Ndesamburo kwa ajili ya maandalizi ya mazishi yake.
Ndugu na Baadhi ya watoto wa marehemu Philemoni Ndesamburo wakiwa katika kikao hicho.
Baadhi ya Viongozi wa Chadema wakishiriki katika kikao hicho.
Baadhi ya watoto wa marehemu Philemoni Ndesamburo.
Baadhi ya Wabunge wakishiriki katika kikao hicho.
Baadhi ya wanandugu wa familia ya marehemu Ndesamburo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...