Mdau Emmanuela Mtatifikolo Kaganda akifurahia baada ya kulamba nondozzz ya Afya ya Umma (Masters of Public Health) toka City University of New York - Graduate school of Public Health kwenye sherehe zilizofanyika katika ukumbi maarufu duniani wa Apollo Theater kitongoji cha Harlem 125th West, jijini New York mapema mwezi huu.
Mdau Emmanuela Kaganda akifurahia pamoja na Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa Mhe. Balozi Modest J. Mero na mkewe
Emmanuela Kaganda akiwa na marafiki zake kwenye sherehe hiyo.
Tabasamu mubashara la ushindi baada ya kula nondozzzzz kwa taswira zaidi jitiririshe hapa chini kiroho saf
Emmanuela Kaganda akiwa kwenye viti vyekundu ndani ya ukumbi maarufu sana New York City na Marekani Apollo Theater, hapa ndipo sherehe zilifanyika.
Emmanuela Kaganda akiwa kwenye kisiki cha 'Ngekewa' ndani ya ukumbi wa Apollo. Kisiki hiki kina sifa ya kukupatia bahati kwenye maisha yako pale unapokigusa ukiwa na maombi ya kutaka kufanikiwa kwa imani ya unachokifanya au kukitarajia katika ndoto zako.
|
Home
Unlabelled
MDAU EMMANUELA KAGANDA ALA NONDOZZZZ YA MASTERS YA AFYA YA UMMA. A.K.A PUBLIC HEALTH)
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...